< Wimbo wa Sulemani 6 >

1 Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mzuri kupita wanawake wote? Mpenzi wako amegeukia njia ipi, tupate kumtafuta pamoja nawe?
Where has your beloved gone, most beautiful among women? In what direction has your beloved gone, so that we may seek him with you?
2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake, kwenye vitalu vya vikolezo, kujilisha bustanini na kukusanya yungiyungi.
My beloved has gone down to his garden, to the beds of spices, to graze in the garden and to gather lilies.
3 Mimi ni wake mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu; yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
I am my beloved's, and my beloved is mine; he grazes among the lilies with pleasure.
4 Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa, upendezaye kama Yerusalemu, umetukuka kama jeshi lenye bendera.
You are as beautiful as Tirzah, my love, as lovely as Jerusalem, as awe-inspiring as an army with its banners.
5 Uyageuze macho yako mbali nami, yananigharikisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoteremka kutoka Gileadi.
Turn your eyes away from me, for they overwhelm me. Your hair is like a flock of goats going down from the slopes of Gilead.
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Your teeth are like a flock of ewes coming up from the washing place. Each one has a twin, and none among them is bereaved.
7 Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
Your cheeks are like pomegranate halves behind your veil.
8 Panaweza kuwepo malkia sitini, masuria themanini na mabikira wasiohesabika;
There are sixty queens, eighty concubines, and young women without number.
9 lakini hua wangu, mkamilifu wangu, ni wa namna ya pekee, binti pekee kwa mama yake, kipenzi cha yeye aliyemzaa. Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa; malkia na masuria walimsifu.
My dove, my undefiled, is the only one; she is the only daughter of her mother; she is the favorite one of the woman who bore her. The young women saw her and called her blessed; the queens and the concubines saw her also, and they praised her:
10 Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko, mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua, ametukuka kama nyota zifuatanazo?
“Who is this who appears like the dawn, as beautiful as the moon, as bright as the sun, as awe-inspiring as an army with its banners?”
11 Niliteremka kwenye bustani ya miti ya milozi ili kutazama machipuko ya bondeni, kuona kama mizabibu imechipua au kama mikomamanga imechanua maua.
I went down into the grove of nut trees to see the young growth in the valley, to see whether the vines had budded, and whether the pomegranates were in bloom.
12 Kabla sijangʼamua, shauku yangu iliniweka katikati ya magari ya kifalme ya kukokotwa na farasi ya watu wangu.
I was so happy that I felt I was riding in the chariot of a prince.
13 Rudi, rudi, ee Mshulami; rudi, rudi ili tupate kukutazama! Mpenzi Kwa nini kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?
Turn back, turn back, you perfect woman; turn back, turn back so that we may gaze on you. The woman speaking to the friends Why do you gaze on the perfect woman, as if on the dance between two armies?

< Wimbo wa Sulemani 6 >