< Wimbo wa Sulemani 6 >
1 Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mzuri kupita wanawake wote? Mpenzi wako amegeukia njia ipi, tupate kumtafuta pamoja nawe?
[[Lad.]] Whither is thy beloved gone, thou fairest among women? Whither hath thy beloved betaken himself? That we may seek him with thee.
2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake, kwenye vitalu vya vikolezo, kujilisha bustanini na kukusanya yungiyungi.
[[M.]] My beloved is gone down to his garden, To the beds of balsam, To feed in the gardens, And to gather lilies.
3 Mimi ni wake mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu; yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
I am my beloved's, and my beloved is mine; He feedeth among the lilies.
4 Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa, upendezaye kama Yerusalemu, umetukuka kama jeshi lenye bendera.
Beautiful art thou, my love, as Tirzah, Lovely as Jerusalem; But terrible as an army with banners.
5 Uyageuze macho yako mbali nami, yananigharikisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoteremka kutoka Gileadi.
Turn away thine eyes from me! They overpower me! Thy locks are like a flock of goats, Which lie down upon Gilead.
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Thy teeth are like a flock of sheep, Which come up from the washing-place, Of which every one hath twins, And none is barren among them.
7 Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
As a divided pomegranate Are thy cheeks behind thy veil.
8 Panaweza kuwepo malkia sitini, masuria themanini na mabikira wasiohesabika;
Threescore are the queens, and fourscore the concubines, And the maidens without number.
9 lakini hua wangu, mkamilifu wangu, ni wa namna ya pekee, binti pekee kwa mama yake, kipenzi cha yeye aliyemzaa. Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa; malkia na masuria walimsifu.
But my dove, my undefiled, is the one; She is the incomparable one of her mother, The darling of her that bore her. The daughters saw her, and blessed her; The queens and concubines, and they praised her.
10 Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko, mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua, ametukuka kama nyota zifuatanazo?
[[Lov.]] Who is this that looketh forth like the morning, Fair as the moon, bright as the sun, And terrible as an army with banners?
11 Niliteremka kwenye bustani ya miti ya milozi ili kutazama machipuko ya bondeni, kuona kama mizabibu imechipua au kama mikomamanga imechanua maua.
[[M.]] I went down into the garden of nuts, To see the green plants of the valley, To see whether the vine blossomed, And the pomegranates budded.
12 Kabla sijangʼamua, shauku yangu iliniweka katikati ya magari ya kifalme ya kukokotwa na farasi ya watu wangu.
Or ever I was aware, My soul had made me like the chariots of the prince's train.
13 Rudi, rudi, ee Mshulami; rudi, rudi ili tupate kukutazama! Mpenzi Kwa nini kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?
[[Lad.]] Return, return, O Shulamite! Return, return, that we may look upon thee! [[M.]] Why should ye look upon the Shulamite, As upon a dance of the hosts?