< Wimbo wa Sulemani 6 >
1 Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mzuri kupita wanawake wote? Mpenzi wako amegeukia njia ipi, tupate kumtafuta pamoja nawe?
Whither is thy friend gone, O fairest of women? whither hath thy friend turned himself? that we may seek him with thee?—
2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake, kwenye vitalu vya vikolezo, kujilisha bustanini na kukusanya yungiyungi.
My beloved is gone down to his garden, to the beds of spices, to feed in the gardens, and to gather lilies.
3 Mimi ni wake mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu; yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
I am my friend's, and my friend is mine: he that feedeth among the lilies.—
4 Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa, upendezaye kama Yerusalemu, umetukuka kama jeshi lenye bendera.
Thou art beautiful, O my beloved, like Thirzah, comely like Jerusalem, terrible as armies encamped round their banners.
5 Uyageuze macho yako mbali nami, yananigharikisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoteremka kutoka Gileadi.
Turn away thy eyes from me, for they have excited me: thy hair is like a flock of goats that come quietly down from mount Gil'ad.
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Thy teeth are like a flock of ewes which are come up from the washing, all of which bear twins, and there is not one among them that is deprived of her young.
7 Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
Like the half of the pomegranate is the upper part of thy cheek behind thy vail.
8 Panaweza kuwepo malkia sitini, masuria themanini na mabikira wasiohesabika;
Sixty are the queens, and eighty the concubines, and the young women without number;
9 lakini hua wangu, mkamilifu wangu, ni wa namna ya pekee, binti pekee kwa mama yake, kipenzi cha yeye aliyemzaa. Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa; malkia na masuria walimsifu.
But one alone is my dove, my guiltless one; she is the only one of her mother, she is the chosen of her that bore her: maidens see her, and call her happy; yea, queens and concubines, and praise her.
10 Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko, mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua, ametukuka kama nyota zifuatanazo?
Who is this that shineth forth like the morning-dawn, beautiful as the moon, bright as the sun, terrible as armies encamped round their banners?
11 Niliteremka kwenye bustani ya miti ya milozi ili kutazama machipuko ya bondeni, kuona kama mizabibu imechipua au kama mikomamanga imechanua maua.
Into the nut-garden was I gone down, to look about among the plants of the valley, to see whether the vine had blossomed, whether the pomegranates had budded.
12 Kabla sijangʼamua, shauku yangu iliniweka katikati ya magari ya kifalme ya kukokotwa na farasi ya watu wangu.
I knew not [how it was], my soul made me [like] the chariots of my noble people.
13 Rudi, rudi, ee Mshulami; rudi, rudi ili tupate kukutazama! Mpenzi Kwa nini kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?
Return, return, O Shulammith; return, return, that we may look upon thee. “What will ye see in the Shulammith?” As though it were the dance of a double company.