< Wimbo wa Sulemani 6 >

1 Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mzuri kupita wanawake wote? Mpenzi wako amegeukia njia ipi, tupate kumtafuta pamoja nawe?
Chorus to Bride: Where has your beloved gone, O most beautiful among women? To where has your beloved turned aside, so that we may seek him with you?
2 Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake, kwenye vitalu vya vikolezo, kujilisha bustanini na kukusanya yungiyungi.
Bride: My beloved has descended to his garden, to the courtyard of aromatic plants, in order to pasture in the gardens and gather the lilies.
3 Mimi ni wake mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu; yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
I am for my beloved, and my beloved is for me. He pastures among the lilies.
4 Wewe ni mzuri, mpenzi wangu, kama Tirsa, upendezaye kama Yerusalemu, umetukuka kama jeshi lenye bendera.
Groom to Bride: My love, you are beautiful: sweet and graceful, like Jerusalem; terrible, like an army in battle array.
5 Uyageuze macho yako mbali nami, yananigharikisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoteremka kutoka Gileadi.
Avert your eyes from me, for they have caused me to fly away. Your hair is like a flock of goats, which have appeared out of Gilead.
6 Meno yako ni kama kundi la kondoo watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Your teeth are like a flock of sheep, which have ascended from the washing, each one with its identical twin, and not one among them is barren.
7 Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
Like the skin of a pomegranate, so are your cheeks, except for your hiddenness.
8 Panaweza kuwepo malkia sitini, masuria themanini na mabikira wasiohesabika;
There are sixty queens, and eighty concubines, and maidens without number.
9 lakini hua wangu, mkamilifu wangu, ni wa namna ya pekee, binti pekee kwa mama yake, kipenzi cha yeye aliyemzaa. Wanawali walimwona na kumwita aliyebarikiwa; malkia na masuria walimsifu.
One is my dove, my perfect one. One is her mother; elect is she who bore her. The daughters saw her, and they proclaimed her most blessed. The queens and concubines saw her, and they praised her.
10 Ni nani huyu atokeaye kama mapambazuko, mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua, ametukuka kama nyota zifuatanazo?
Chorus to Groom: Who is she, who advances like the rising dawn, as beautiful as the moon, as elect as the sun, as terrible as an army in battle array?
11 Niliteremka kwenye bustani ya miti ya milozi ili kutazama machipuko ya bondeni, kuona kama mizabibu imechipua au kama mikomamanga imechanua maua.
Bride: I descended to the garden of nuts, in order to see the fruits of the steep valleys, and to examine whether the vineyard had flourished and the pomegranates had produced buds.
12 Kabla sijangʼamua, shauku yangu iliniweka katikati ya magari ya kifalme ya kukokotwa na farasi ya watu wangu.
I did not understand. My soul was stirred up within me because of the chariots of Amminadab.
13 Rudi, rudi, ee Mshulami; rudi, rudi ili tupate kukutazama! Mpenzi Kwa nini kumtazama Mshulami, kama kutazama ngoma ya Mahanaimu?
Chorus to Bride: Return, return, O Sulamitess. Return, return, so that we may consider you. Chorus to Groom: What will you see in the Sulamitess, other than choruses of encampments?

< Wimbo wa Sulemani 6 >