< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
Przyszedłem do ogrodu mego, siostro moja, oblubienico moja! zbieram myrrę moję z rzeczami wonnemi mojemi; jem plastr mój z miodem moim, piję wino moje z mlekiem mojem. Jedzcież, przyjaciele! pijcie, a pijcie dostatkiem, mili moi!
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Jać śpię; ale serce moje czuje, i słyszy głos miłego mego, kołaczącego i mówiącego: Otwórz mi, siostro moja, przyjaciółko moja, gołębico moja, uprzejma moja! albowiem głowa moja pełna jest rosy, a kędzierze moje kropli nocnych.
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
I odpowiedziałem: Zewlekłam suknię moję, jakoż ją oblec mam? umyłam nogi moje, jakoż je zmazać mam?
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
Miły mój ściągnął rękę swoję dziurą, a wnętrzności moje wzruszyły się we mnie.
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
I wstałam, abym otworzyła miłemu memu, a oto z rąk mych kapała myrra, a z palców moich myrra ciekąca na rękojeść zawory.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
Otworzyłam miłemu memu; ale miły mój już był odszedł i minął. Omdlałam była na głos jego; szukałam go, alem go nie znalazła; wołałam go, ale mi się nieozwał.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
Natrafili mię stróże, co chodzą po mieście; ubili mię, zranili mię, wzięli i płaszcz mój ze mnie stróże murów.
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
Poprzysięgam was, córki Jeruzalemskie! Jeślibyście znalazły miłego mego, abyście mu powiedziały, żem od miłości zachorowała.
9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
Cóż ma miły twój nad innych miłych, o najpiękniejsza między niewiastami? co ma miły twój nad innych miłych, że nas tak poprzysięgasz?
10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
Miły mój biały i rumiany, i zacniejszy nad innych dziesięć tysięcy.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
Głowa jego jako bryła szczerego złota; włosy jego kędzierzawe, czarne jako kruk;
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
Oczy jego jako gołębicy nad strumieniami wody, jako umyte w mleku, stojące w mierze swojej;
13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
Policzki jego jako zagonki ziół wonnych, jako kwiatki wonnych rzeczy; wargi jego jako lilije wypuszczające myrrę ciekącą;
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
Ręce jego jako pierścienie złote, osadzone drogim kamieniem, hiacyntem; brzuch jego jako glanc kości słoniowej, safirem osadzonej;
15 Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
Golenie jego jako słupy marmurowe, postawione na podstawkach złota wybornego; oblicze jego jako Liban, wyborne jako cedry;
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
Usta jego nader słodkie, a wszystek jest pożądany. Taki ci jest miły mój, i taki przyjaciel mój, o córki Jeruzalemskie!

< Wimbo wa Sulemani 5 >