< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
"Minä tulen yrttitarhaani, siskoni, morsiameni; minä poimin mirhani ja balsamini, minä syön mesileipäni ja hunajani, juon viinini ja maitoni." Syökää, ystävät, juokaa ja juopukaa rakkaudesta.
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Minä nukuin, mutta minun sydämeni valvoi. Kuule, rakkaani kolkuttaa: "Avaa minulle, siskoseni, armaani, kyyhkyseni, puhtoiseni. Sillä pääni on kastetta täynnä, kiharani yön pisaroita."
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
"Olen ihokkaani riisunut; pukisinko sen päälleni enää? Olen jalkani pessyt; tahraisinko ne taas?"
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
Rakkaani pisti kätensä ovenreiästä sisään. Silloin minun sydämeni liikkui häntä kohden;
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
minä nousin avaamaan rakkaalleni, ja minun käteni tiukkuivat mirhaa, sormeni sulaa mirhaa salvan kädensijoihin.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
Minä avasin rakkaalleni, mutta rakkaani oli kadonnut, mennyt menojaan. Hänen puhuessaan oli sieluni vallannut hämmennys. Minä etsin häntä, mutta en häntä löytänyt; minä huusin häntä, mutta ei hän minulle vastannut.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
Kohtasivat minut vartijat, jotka kaupunkia kiertävät, he löivät minua ja haavoittivat minut; päällysharson riistivät yltäni muurien vartijat.
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
"Minä vannotan teitä, te Jerusalemin tyttäret: jos löydätte rakkaani, mitä hänelle sanotte? Sanokaa, että minä olen rakkaudesta sairas."
9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
"Mitä on sinun rakkaasi muita parempi, sinä naisista kaunein? Mitä on sinun rakkaasi muita parempi, ettäs meitä näin vannotat?"
10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
"Minun rakkaani on valkoinen ja punainen, kymmentä tuhatta jalompi.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
Hänen päänsä on kultaa, puhtainta kultaa, hänen kiharansa kuin palmunlehvät, mustat kuin kaarne.
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
Hänen silmänsä ovat kuin kyyhkyset vesipurojen partaalla, jotka ovat maidossa kylpeneet ja istuvat runsauden ääressä.
13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
Hänen poskensa ovat kuin balsamilava, kuin höystesäiliöt; hänen huulensa ovat liljat, ne tiukkuvat sulaa mirhaa.
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
Hänen käsivartensa ovat kultatangot, krysoliittejä täynnä. Hänen lantionsa on norsunluinen taideteos, safiireilla peitetty.
15 Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
Hänen jalkansa ovat marmoripatsaat aitokultaisten jalustain nojassa. Hän on näöltänsä kuin Libanon, uhkea kuin setripuut.
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
Hänen suunsa on sula makeus, hän on pelkkää suloisuutta. Sellainen on minun rakkaani, sellainen on ystäväni, te Jerusalemin tyttäret."

< Wimbo wa Sulemani 5 >