< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
[[Lov.]] I am come to my garden, my sister, my spouse! I gather my myrrh with my balsam, I eat my honeycomb with my honey, I drink my wine with my milk. Eat, O friends! Drink, yea, drink abundantly, my loved companions!
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
[[M.]] I slept, but my heart was awake; It was the voice of my beloved, who was knocking: “Open to me, my sister, my love, My dove, my perfect one! For my head is filled with dew, And my locks with the drops of the night.”
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
“I have taken off my vest [[said I]]; How shall I put it on? I have washed my feet; How shall I soil them?”
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
My beloved put in his hand by the hole of the door, And my heart was moved for him.
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
I rose up to open to my beloved, And my hands dropped with myrrh, And my fingers with self-flowing myrrh, upon the handles of the bolt.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
I opened to my beloved; But my beloved had withdrawn himself, and was gone. I was not in my senses while he spake with me! I sought him, but could not find him; I called him, but he gave me no answer.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
The watchmen that go about the city found me; They smote me, they wounded me; The keepers of the walls took away from me my veil.
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
I charge you, O ye daughters of Jerusalem! If ye should find my beloved, —What will ye tell him? That I am sick with love.
9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
[[Lad.]] What is thy beloved more than another beloved, O thou fairest among women! What is thy beloved more than another beloved, That thus thou dost charge us?
10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
[[M.]] My beloved is white and ruddy, The chief among ten thousand.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
His head is as the most fine gold; His locks waving palm-branches, Black as a raven;
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
His eyes are doves by streams of water, Washed with milk, dwelling in fulness;
13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
His cheeks are like a bed of balsam, Like beds of spices; His lips are lilies Dropping self-flowing myrrh;
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
His hands are gold rings set with chrysolite; His body is wrought-work of ivory, overlaid with sapphires;
15 Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
His legs are marble pillars, resting on pedestals of fine gold; His aspect is like Lebanon, Majestic like the cedars;
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
His mouth is sweetness; His whole being, loveliness. This is my beloved, This my friend, O ye daughters of Jerusalem!

< Wimbo wa Sulemani 5 >