< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
I enter my garden, my sister, my bride! I gather myrrh with my spice. I eat my honeycomb with my honey. I drink wine with my milk. Let us eat our fill of love! Let us be drunk with love!
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Though I was asleep, my mind was racing. I heard my love knocking, and calling out, “Please open the door, my sister, my darling, my dove, my perfect love. My head is soaked with dew, my hair is wet from the night mist.”
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
I replied, “I've already got undressed. I don't have to get dressed again, do I? I've already washed my feet. I don't have to make them dirty again, do I?”
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
My love thrust his hand into the opening. Deep inside I longed for him.
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
I got up to let my love in. My hands dripped with myrrh, my fingers with liquid myrrh, as I grabbed the handles of the bolt.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
I opened up to my love, but he had left—he was gone! I was crushed as a result. I looked for him but I couldn't find him. I called him but he didn't answer.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
The watchmen found me as they went through the city. They beat me, they hurt me, and stole my cloak, those watchmen of the walls.
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
Women of Jerusalem, promise me if you find my love and wonder what you should tell him, tell him I am weak with love.
9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
Why is the one you love better than any other, most beautiful of women? In what way is the one you love better than any other that we should promise you that?
10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
My love has dazzling good looks and is very fit—better than ten thousand others!
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
His head is like the finest gold, his hair is wavy and black as the raven.
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
His eyes are like doves beside springs of water, washed with milk and mounted like sparkling jewels.
13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
His cheeks are like a flowerbed of spices that produces fragrance. His lips are like lilies, dripping with liquid myrrh.
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
His arms are round bars of gold inlaid with jewels. His abdomen is like carved ivory inlaid with lapis lazuli.
15 Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
His legs are columns of alabaster set on bases of gold. He looks strong, like the mighty cedars of Lebanon.
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
His mouth is the sweetest ever; he is totally desirable! This is my love, my friend, women of Jerusalem.

< Wimbo wa Sulemani 5 >