< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
Bride: May my beloved enter into his garden, and eat the fruit of his apple trees. Groom to Bride: I have arrived in my garden, O my sister, my spouse. I have harvested my myrrh, with my aromatic oils. I have eaten the honeycomb with my honey. I have drunk my wine with my milk. Eat, O friends, and drink, and be inebriated, O most beloved.
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Bride: I sleep, yet my heart watches. The voice of my beloved knocking: Groom to Bride: Open to me, my sister, my love, my dove, my immaculate one. For my head is full of dew, and the locks of my hair are full of the drops of the night.
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
Bride: I have taken off my tunic; how shall I be clothed in it? I have washed my feet; how shall I spoil them?
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
My beloved put his hand through the window, and my inner self was moved by his touch.
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
I rose up in order to open to my beloved. My hands dripped with myrrh, and my fingers were full of the finest myrrh.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
I opened the bolt of my door to my beloved. But he had turned aside and had gone away. My soul melted when he spoke. I sought him, and did not find him. I called, and he did not answer me.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
The keepers who circulate through the city found me. They struck me, and wounded me. The keepers of the walls took my veil away from me.
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
I bind you by oath, O daughters of Jerusalem, if you find my beloved, announce to him that I languish through love.
9 Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
Chorus to Bride: What kind of beloved is your beloved, O most beautiful among women? What kind of beloved is your beloved, so that you would bind us by oath?
10 Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
Bride: My beloved is white and ruddy, elect among thousands.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
His head is like the finest gold. His locks are like the heights of palm trees, and as black as a raven.
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
His eyes are like doves, which have been washed with milk over rivulets of waters, and which reside near plentiful streams.
13 Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
His cheeks are like a courtyard of aromatic plants, sown by perfumers. His lips are like lilies, dripping with the best myrrh.
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
His hands are smoothed gold, full of hyacinths. His abdomen is ivory, accented with sapphires.
15 Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
His legs are columns of marble, which have been established over bases of gold. His appearance is like that of Lebanon, elect like the cedars.
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
His throat is most sweet, and he is entirely desirable. Such is my beloved, and he is my friend, O daughters of Jerusalem.

< Wimbo wa Sulemani 5 >