< Wimbo wa Sulemani 4 >

1 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, jinsi ulivyo mzuri! Macho yako nyuma ya shela yako ni kama ya hua. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi zikishuka kutoka Mlima Gileadi.
تو چه زیبایی، ای محبوبهٔ من! چشمانت از پشت روبند به زیبایی و لطافت کبوتران است. گیسوان مواج تو مانند گلهٔ بزهاست که از کوه جلعاد سرازیر می‌شوند.
2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi, watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
دندانهای تو به سفیدی گوسفندانی هستند که به تازگی پشمشان را چیده و آنها را شسته باشند؛ هر کدام جفت خویش را دارد و هیچ‌کدام تنها نیست.
3 Midomo yako ni kama uzi mwekundu, kinywa chako kinapendeza. Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
لبانت سرخ و دهانت زیباست. گونه‌هایت از پشت روبند همانند دو نیمهٔ انار است.
4 Shingo yako ni kama mnara wa Daudi, uliojengwa kwa madaha, juu yake zimetundikwa ngao elfu, zote ni ngao za mashujaa.
گردنت به گردی برج داوود است و زینت گردنت مانند هزار سپر سربازانی است که دور تا دور برج را محاصره کرده‌اند.
5 Matiti yako mawili ni kama wana-paa wawili, kama wana-paa mapacha wajilishao katikati ya yungiyungi.
سینه‌هایت مثل بچه غزالهای دو قلویی هستند که در میان سوسنها می‌چرند.
6 Hata kupambazuke na vivuli vikimbie, nitakwenda kwenye mlima wa manemane na kwenye kilima cha uvumba.
پیش از آنکه آفتاب طلوع کند و سایه‌ها بگریزند، من به کوه مُر و تپهٔ کندر خواهم رفت.
7 Wewe ni mzuri kote, mpenzi wangu, hakuna hitilafu ndani yako.
تو چه زیبایی، ای محبوبهٔ من! در تو هیچ نقصی نیست.
8 Enda nami kutoka Lebanoni, bibi arusi wangu, enda nami kutoka Lebanoni. Shuka kutoka ncha ya Amana, kutoka juu ya Seniri, kilele cha Hermoni, kutoka mapango ya simba na kutoka mlima wapendapo kukaa chui.
ای عروس من، با من بیا. از بلندیهای لبنان، از قلۀ اَمانه و از فراز سنیر و حرمون، جایی که شیران و پلنگان لانه دارند، به زیر بیا.
9 Umeiba moyo wangu, dada yangu, bibi arusi wangu; umeiba moyo wangu kwa mtazamo mmoja wa macho yako, kwa kito kimoja cha mkufu wako.
ای محبوبهٔ من و ای عروس من، تو با یک نگاهت دلم را ربودی و با یک حلقهٔ گردنبندت مرا در بند کشیدی.
10 Tazama jinsi pendo lako linavyofurahisha, dada yangu, bibi arusi wangu! Pendo lako linafurahisha aje zaidi ya divai, na harufu ya manukato yako zaidi ya kikolezo chochote!
ای محبوبهٔ من و ای عروس من، چه گواراست عشق تو! عشق تو دلپذیرتر از شراب است و خوشبوتر از تمامی عطرها.
11 Midomo yako inadondosha utamu kama sega la asali, bibi arusi wangu; maziwa na asali viko chini ya ulimi wako. Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ile ya Lebanoni.
از لبان تو عسل می‌چکد و در زیر زبانت شیر و عسل نهفته است. بوی لباس تو همچون رایحهٔ دل‌انگیز درختان لبنان است.
12 Wewe ni bustani iliyofungwa, dada yangu, bibi arusi wangu; wewe ni chanzo cha maji kilichozungushiwa kabisa, chemchemi yangu peke yangu.
ای محبوبهٔ من و ای عروس من، تو مانند باغی بسته، و همچون چشمه‌ای دست نیافتنی، تنها از آن من هستی.
13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga yenye matunda mazuri sana, yenye hina na nardo,
تو مثل بوستان زیبای انار هستی که در آن میوه‌های خوش طعم به ثمر می‌رسند. در تو سنبل و حنا، زعفران و نیشکر، دارچین و گیاهان معطری چون مُر و عود می‌رویند.
14 nardo na zafarani, mchai na mdalasini, pamoja na kila aina ya mti wa uvumba, manemane na udi, na aina zote za vikolezo bora kuliko vyote.
15 Wewe ni chemchemi ya bustani, kisima cha maji yatiririkayo, yakitiririka kutoka Lebanoni.
تو مانند چشمه‌ساری هستی که باغها را سیراب می‌کند و همچون آب روانی هستی که از کوههای لبنان جاری می‌شود.
16 Amka, upepo wa kaskazini, na uje, upepo wa kusini! Vuma juu ya bustani yangu, ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ngʼambo. Mpendwa wangu na aje bustanini mwake na kuonja matunda mazuri sana.
ای نسیم شمال، و ای باد جنوب، برخیزید! برخیزید و بر من که باغ محبوبم هستم بوزید تا بوی خوش من همه جا پراکنده شود. بگذارید او به باغ خود بیاید و از میوه‌های خوش طعم آن بخورد.

< Wimbo wa Sulemani 4 >