< Wimbo wa Sulemani 4 >

1 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, jinsi ulivyo mzuri! Macho yako nyuma ya shela yako ni kama ya hua. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi zikishuka kutoka Mlima Gileadi.
Moulang: Namelhoi ngeije, ngainu, seidoh jou hoi hilouvin nahoi ngeije. Na ponlukhuh noija namit teni vakhu abang jeng’e. Nasam kailha jong Gilead lhang dunga kon kel-hon hung kijot suh abang jeng’e.
2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi, watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Naha ho kelngoi kihet ngousel jouchet’na kisop thengsel bang in akangleh jeng’e. Na mehiuheo dan nolnabei ahin, na hatu jouse jong akigol khom dildel uve.
3 Midomo yako ni kama uzi mwekundu, kinywa chako kinapendeza. Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
Nane geiteni jong patsandup abangin, nakam jeng jong mihiptah ahi. Na bengmai langto jong na ponlukhuh noijah kolbuthei chang asan jit jet abang jenge.
4 Shingo yako ni kama mnara wa Daudi, uliojengwa kwa madaha, juu yake zimetundikwa ngao elfu, zote ni ngao za mashujaa.
Na ngongchang jong David insang, migal-hang asang aja galmanchah-omphoa kijem pah jeng toh abangin avet-hoi ngeije.
5 Matiti yako mawili ni kama wana-paa wawili, kama wana-paa mapacha wajilishao katikati ya yungiyungi.
Na-ang teni jong sapengnou teni, Lily pah lah-a lhale sapengnou pengkop teni abange.
6 Hata kupambazuke na vivuli vikimbie, nitakwenda kwenye mlima wa manemane na kwenye kilima cha uvumba.
Khovahkon huilhi nun masang, jan muthim lim kiheimang masang ah; keiman Myrrh molsang kajot’na, bego lhangdung ka jot touding ahitai.
7 Wewe ni mzuri kote, mpenzi wangu, hakuna hitilafu ndani yako.
Nangma na pumpin nahoije, ngainu, na hoi chamkim ngeiye.
8 Enda nami kutoka Lebanoni, bibi arusi wangu, enda nami kutoka Lebanoni. Shuka kutoka ncha ya Amana, kutoka juu ya Seniri, kilele cha Hermoni, kutoka mapango ya simba na kutoka mlima wapendapo kukaa chui.
Lebanon’a kon in neihin juiyin, ka deilhennu, neihin jui tan Lebanon’a kon in. Senir le Hermon molvum, keipi-bahkai ho kokhuh umna lah, Kei-ahsite chenna lhang, hin juisuh-in Amana Molsanga kon’in hung kumsuh tan.
9 Umeiba moyo wangu, dada yangu, bibi arusi wangu; umeiba moyo wangu kwa mtazamo mmoja wa macho yako, kwa kito kimoja cha mkufu wako.
Nang in ka lungsung na lodim in, ka goulu nahi, kangai ka jiding nu. Na khivui val emsel toh namit-ha’a neivet dan in ei hentang den jeng tai.
10 Tazama jinsi pendo lako linavyofurahisha, dada yangu, bibi arusi wangu! Pendo lako linafurahisha aje zaidi ya divai, na harufu ya manukato yako zaidi ya kikolezo chochote!
Nei ngailutnan ei kipa thanop sah-e, ka goulu nahi; ka ngai kaji ding nu. Nei ngaina hi lengpitwi sang in alhumjon, na gimnamtwi hi pahnamtwi sang in jong atwi joi.
11 Midomo yako inadondosha utamu kama sega la asali, bibi arusi wangu; maziwa na asali viko chini ya ulimi wako. Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ile ya Lebanoni.
Na negei teni khoiju sang in alhum joi, O ka ji ding nu. Nalei noija khoiju le bongnoi aume. Na von jouse jong Lebanon lhangpah gimtwi anam’e.
12 Wewe ni bustani iliyofungwa, dada yangu, bibi arusi wangu; wewe ni chanzo cha maji kilichozungushiwa kabisa, chemchemi yangu peke yangu.
Nangma hi keija ding monga pahcha lei, goulu, chongmou chule khal laiya twinah kiselguh tobang nahi.
13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga yenye matunda mazuri sana, yenye hina na nardo,
Na pheichung jong kolbuthei toh muinam kikhat tah henna,
14 nardo na zafarani, mchai na mdalasini, pamoja na kila aina ya mti wa uvumba, manemane na udi, na aina zote za vikolezo bora kuliko vyote.
Chule leipah namtwi toh sehlhum, kolju le thingthal, bego le Myrhh, aloe le muinam jouse dinga kingapna ahi.
15 Wewe ni chemchemi ya bustani, kisima cha maji yatiririkayo, yakitiririka kutoka Lebanoni.
Nangma honlei twinah, twichim twikul; Lebanon lhanga kon hung longlha tobang nahi.
16 Amka, upepo wa kaskazini, na uje, upepo wa kusini! Vuma juu ya bustani yangu, ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ngʼambo. Mpendwa wangu na aje bustanini mwake na kuonja matunda mazuri sana.
Mounu: Khang in, Sahlam khohui! thouvin, lhanglam khohui! Ka honlei jon ah hung nung in lang akimvel jouse agimtwi hi lhutsohhel tan. O ka goldeipa, na honleija hin hunglut in lang, theiga hoipen hung kilon lang, hung nen.

< Wimbo wa Sulemani 4 >