< Wimbo wa Sulemani 3 >

1 Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
L’Épouse. Sur ma couche, pendant les nuits, j’ai cherché celui que chérit mon âme; je l’ai cherché et ne l’ai pas trouvé.
2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
Je me lèverai, et je ferai le tour de la cité: dans les bourgs et les places publiques, je chercherai celui que chérit mon âme; je l’ai cherché et ne l’ai pas trouvé.
3 Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
Elles m’ont rencontrée, les sentinelles qui gardent la cité: Celui que chérit mon âme, est-ce que vous ne l’avez pas vu?
4 Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
Lorsque je les ai eu un peu dépassées, j’ai rencontré celui que chérit mon âme: je l’ai saisi et je ne le laisserai pas aller, jusqu’à ce que je l’introduise dans la maison de ma mère, et dans la chambre de celle qui m’a donné le jour.
5 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
L’Époux. Je vous conjure, filles de Jérusalem, par les chevreuils et les cerfs des campagnes, ne dérangez pas, et ne réveillez pas la bien-aimée, jusqu’à ce qu’elle-même le veuille.
6 Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
Les filles de Jérusalem. Quelle est celle-ci, qui monte par le désert comme une colonne de fumée d’aromates de myrrhe, d’encens, et de toutes sortes de poudres de parfums?
7 Tazama! Ni gari la Solomoni lisindikizwalo na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
Voici la couche de Salomon: soixante vaillants guerriers des plus vaillants d’Israël l’environnent,
8 wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.
Tous portant des glaives et très habiles dans les combats; chacun a son glaive sur sa cuisse, à cause des craintes de la nuit.
9 Mfalme Solomoni alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
Le roi Salomon s’est fait une litière de bois du Liban;
10 Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
Il en a fait les colonnes d’argent, le dossier d’or, le siège de pourpre: le milieu, il l’a couvert de ce qu’il y a de plus précieux à cause des filles de Jérusalem.
11 Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.
Sortez et voyez, filles de Sion, le roi Salomon avec le diadème dont le couronna sa mère au jour de ses noces, et au jour de la joie de son cœur.

< Wimbo wa Sulemani 3 >