< Wimbo wa Sulemani 3 >

1 Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
By night on my bed I sought him whom my soul loves. I sought him, but I did not find him.
2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
I said, I will rise now, and go around the city. In the streets and in the broad ways I will seek him whom my soul loves. I sought him, but I did not find him.
3 Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
The watchmen who go about the city found me. I said, Did ye see him whom my soul loves?
4 Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
It was but a little that I passed from them when I found him whom my soul loves. I held him, and would not let him go until I had brought him into my mother's house, and into the chamber of her who conceived me.
5 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
I adjure you, O daughters of Jerusalem, by the roes, or by the hinds of the field, that ye stir not up, nor awake love, until it please.
6 Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
Who is this who comes up from the wilderness like pillars of smoke, perfumed with myrrh and frankincense, with all powders of the merchant?
7 Tazama! Ni gari la Solomoni lisindikizwalo na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
Behold, it is the litter of Solomon. Sixty mighty men are around it, of the mighty men of Israel.
8 wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.
They all handle the sword, and are expert in war. Every man has his sword upon his thigh, because of fear in the night.
9 Mfalme Solomoni alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
King Solomon made himself a palanquin of the wood of Lebanon.
10 Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
He made the pillars thereof of silver, the bottom thereof of gold, the seat thereof of purple, the midst thereof being paved with love, from the daughters of Jerusalem.
11 Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.
Go forth, O ye daughters of Zion, and behold king Solomon with the crown with which his mother has crowned him in the day of his espousals, and in the day of the gladness of his heart.

< Wimbo wa Sulemani 3 >