< Wimbo wa Sulemani 3 >
1 Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
Po ležaju svome, u noćima, tražila sam onoga koga ljubi duša moja, tražila sam ga, ali ga nisam našla.
2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
Ustat ću dakle i optrčati grad, po ulicama i trgovima tražit ću onoga koga ljubi duša moja: tražila sam ga, ali ga nisam našla.
3 Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
Sretoše me čuvari koji grad obilaze: “Vidjeste li onoga koga ljubi duša moja?”
4 Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
Tek što pođoh od njih, nađoh onoga koga ljubi duša moja. Uhvatila sam ga i neću ga pustiti, dok ga ne uvedem u kuću majke svoje, u ložnicu roditeljke svoje.
5 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
Zaklinjem vas, kćeri jeruzalemske, srnama i košutama poljskim, ne budite, ne budite ljubav moju dok sama ne bude htjela!
6 Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
Što se to diže iz pustinje kao stup dima iz kada smirne i tamjana i svih prašaka mirodijskih?
7 Tazama! Ni gari la Solomoni lisindikizwalo na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
Gle, to je nosiljka Salomonova, oko nje šezdeset kršnih momaka između najkršnijih u Izraelu.
8 wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.
Svi su vični mačevima, za rat su izvježbani, svakome je sablja o boku zbog opasnosti noćnih.
9 Mfalme Solomoni alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
Sebi je prijestolje načinio kralj Salomon od drveta libanskoga.
10 Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
Stupove je napravio od srebra, naslon od zlata, sjedište od grimiza, unutra je sve ukrašeno ljubavlju kćeri jeruzalemskih.
11 Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.
Izađite, kćeri sionske, i vidite kralja Salomona pod dijademom kojim ga mati ovjenčala na dan svadbe njegove, na dan radosti njegova srca.