< Wimbo wa Sulemani 2 >

1 Mimi ni ua la Sharoni, yungiyungi ya bondeni.
Es esmu roze Šaronā un lilija ielejā.
2 Kama yungiyungi katikati ya miiba ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali.
Tā kā lilija starp ērkšķiem, tāda ir mana draudzene starp tām meitām.
3 Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wanaume vijana. Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu, na tunda lake ni tamu kwangu.
Tā kā ābele starp meža kokiem, tāds ir mans draugs starp tiem dēliem. Es ilgojos sēdēt viņa pavēnī, un viņa auglis manai mutei salds.
4 Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu, na bendera ya huyu mwanaume juu yangu ni upendo.
Viņš mani ved vīna namā, un mīlestība ir viņa karogs pār mani.
5 Nitie nguvu kwa zabibu kavu, niburudishe kwa matofaa, kwa maana ninazimia kwa mapenzi.
Atspirdzinājiet mani ar vīna ogām un spēcinājiet mani ar āboliem; jo es nīkstu no mīlestības.
6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kuume unanikumbatia.
Viņa kreisā roka ir apakš manas galvas, un viņa labā roka mani apkampj.
7 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
Es jūs mīļi lūdzu, jūs Jeruzālemes meitas, pie tām stirnām un kalnu kazām laukā, neuztraucat un nemodinājat mīlestību, kamēr tai pašai patīk.
8 Sikiliza! Mpenzi wangu! Tazama! Huyu hapa anakuja, akirukaruka juu milimani akizunguka juu ya vilima.
Šī ir mana drauga balss; redzi, viņš nāk un lēkā pa tiem kalniem un deij pa tiem pakalniem.
9 Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana. Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu, akitazama kupitia madirishani, akichungulia kimiani.
Mans draugs ir līdzīgs stirnai vai jaunam briedim. Redzi, viņš stāv aiz sienas, skatās caur logiem un raugās caur skadriņiem.
10 Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia, “Inuka, mpenzi wangu, mrembo wangu, tufuatane.
Mans draugs atbild un saka uz mani: celies, mana draudzene, mana skaistā, un nāc!
11 Tazama! Wakati wa masika umepita, mvua imekwisha na ikapita.
Jo redzi, ziema ir pagājusi, stiprais lietus jau ir pārgājis un nost.
12 Maua yanatokea juu ya nchi; majira ya kuimba yamewadia, sauti za njiwa zinasikika katika nchi yetu.
Puķes rādās laukā, dziesmu laiks atnācis, un ūbeles balss dzirdama mūsu zemē.
13 Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni, zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri. Inuka, njoo mpenzi wangu. Mrembo wangu, tufuatane.”
Vīģes koks dabūjis pumpurus, un vīna koki plaukst un dod smaržu; celies, nāc, mana draudzene, mana skaistā, nāc šurp!
14 Hua wangu penye nyufa za majabali, mafichoni pembezoni mwa mlima, nionyeshe uso wako, na niisikie sauti yako, kwa maana sauti yako ni tamu, na uso wako unapendeza.
Mans balodis akmeņu kalnos, apslēptos plaisumos, parādi man savu vaigu, dod man savu balsi dzirdēt; jo tava balss ir salda, un tavs vaigs ir mīlīgs.
15 Tukamatie mbweha, mbweha wale wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu, mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua.
Gūstat mums lapsas, tās mazās lapsas, kas vīna dārzus maitā, jo mūsu vīna dārzi stāv ziedos.
16 Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake, yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
Mans draugs ir mans, es esmu viņa, kas pa tām lilijām gana.
17 Mpaka jua linapochomoza, na vivuli vikimbie, rudi, mpenzi wangu, na uwe kama paa, au kama ayala kijana juu ya vilima vya Betheri.
Kamēr diena metās dzestra un ēnas bēg, atgriezies, mans draugs, kā stirna, vai kā jauns briedis pa kalnu plaisumiem.

< Wimbo wa Sulemani 2 >