< Ruth 1 >

1 Wakati Waamuzi walipotawala Israeli, kulikuwa na njaa katika nchi. Mtu mmoja kutoka nchi ya Bethlehemu ya Yuda, pamoja na mke wake na wanawe wawili, akaenda kuishi katika nchi ya Moabu.
And it was in [the] days of [the] judging of the judges and it was a famine in the land and he went a man from Beth-lehem Judah to sojourn in [the] region of Moab he and wife his and [the] two sons his.
2 Mtu huyu aliitwa Elimeleki, mkewe aliitwa Naomi, na hao wanawe wawili waliitwa Maloni na Kilioni. Walikuwa Waefrathi kutoka Bethlehemu ya Yuda. Wakaenda katika nchi ya Moabu, wakaishi huko.
And [the] name of the man [was] Elimelech and [the] name of wife his [was] Naomi and [the] name of [the] two sons his - [was] Mahlon and Kilion Ephrathites from Beth-lehem Judah and they came [the] region of Moab and they were there.
3 Elimeleki mumewe Naomi akafa, hivyo Naomi akabaki na wanawe wawili.
And he died Elimelech [the] husband of Naomi and she was left she and [the] two sons her.
4 Nao wakaoa wanawake Wamoabu, jina la mmoja aliitwa Orpa, na wa pili aliitwa Ruthu. Baada ya kama miaka kumi,
And they took for themselves wives Moabite [the] name of the one [was] Orpah and [the] name of the second [was] Ruth and they dwelt there about ten years.
5 Maloni na Kilioni pia wakafa. Basi Naomi akabaki hana mume wala wanawe wawili.
And they died also both of them Mahlon and Kilion and she was left the woman from both children her and from husband her.
6 Aliposikia akiwa huko Moabu kwamba Bwana amewasaidia watu wake kwa kuwapa chakula, Naomi na wakweze wakajiandaa kurudi nyumbani.
And she arose she and daughters-in-law her and she returned from [the] region of Moab if she had heard in [the] region of Moab that he had visited Yahweh people his by giving to them food.
7 Yeye na wakweze wawili wakaondoka pale walipokuwa wakiishi na kushika njia kurudi nchi ya Yuda.
And she went out from the place where she had been there and [the] two daughters-in-law her [were] with her and they went on the way to return to [the] land of Judah.
8 Ndipo Naomi akawaambia wale wakwe zake wawili, “Rudini, kila mmoja wenu nyumbani kwa mama yake. Bwana na awatendee fadhili kama mlivyowatendea hao waliofariki, na pia mimi.
And she said Naomi to [the] two daughters-in-law her go return [each] woman to [the] house of mother her (may he deal *Q(K)*) Yahweh with you covenant loyalty just as you have dealt with the dead and with me.
9 Bwana na amjalie kila mmoja wenu maisha mema nyumbani kwa mume mwingine.” Kisha akawabusu, nao wakalia kwa sauti kubwa,
May he give Yahweh to you and find rest [each] woman [the] house of husband her and she kissed them and they raised voice their and they wept.
10 wakamwambia, “Tutarudi pamoja na wewe nyumbani kwa watu wako.”
And they said to her that with you we will return to people your.
11 Lakini Naomi akasema, “Rudini nyumbani, binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, mimi nitaweza tena kuwa na wana wengine ambao wataweza kuwaoa ninyi?
And she said Naomi go back O daughters my why? will you go with me ¿ still [belong] to me [do] sons in inward parts my and they will become of you husbands.
12 Rudini nyumbani, binti zangu; mimi ni mzee kiasi kwamba siwezi kumpata mume mwingine. Hata kama ningefikiria kuwa bado kuna tumaini kwangu, hata kama ningekuwa na mume usiku huu na kuwazaa wana,
Go back O daughters my go for I am [too] old for belonging to a husband if I said there for me [is] hope also I belonged this night to a husband and also I bore sons.
13 je, mngesubiri mpaka wakue? Mngebakia bila kuolewa mkiwasubiri? La, hasha, binti zangu. Nimepata uchungu kuliko ninyi, kwa sababu mkono wa Bwana umekuwa kinyume nami!”
¿ Therefore - will you wait until that they will grow up ¿ therefore will you shut yourselves off to not to belong to a husband may not [it be] O daughters my for it is bitter to me very more than you that it has gone forth on me [the] hand of Yahweh.
14 Kisha wakalia tena kwa sauti. Orpa akambusu mama mkwe wake, akaenda zake, lakini Ruthu akaambatana naye.
And they raised voice their and they wept again and she kissed Orpah mother-in-law her and Ruth she clung to her.
15 Naomi akamwambia, “Tazama, mwenzako anarejea kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudi pamoja naye.”
And she said there! she has returned sister-in-law your to people her and to gods her go back after sister-in-law your.
16 Lakini Ruthu akajibu, “Usinisihi nikuache au niache kukufuata. Utakakokwenda nami nitakwenda, na wewe utakapoishi nitaishi. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
And she said Ruth may not you entreat me to abandon you to turn back from after you for to where you will go I will go and at where you will lodge I will lodge people your [will be] people my and God your [will be] God my.
17 Pale utakapofia nami nitafia hapo, na papo hapo nitazikwa. Bwana na aniadhibu vikali, kama kitu kingine chochote kitanitenga nawe isipokuwa kifo.”
At where you will die I will die and there I will be buried thus may he do Yahweh to me and thus may he add if death it will separate between me and between you.
18 Naomi alipotambua kwamba Ruthu amenuia kufuatana naye, hakuendelea kumsihi tena.
And she saw that [was] determined she to go with her and she ceased to speak to her.
19 Kwa hiyo hao wanawake wawili wakaondoka, wakafika Bethlehemu. Walipofika Bethlehemu, mji mzima ulitaharuki, wanawake wakashangaa, wakasema, “Huyu aweza kuwa ni Naomi?”
And they went [the] two of them until came they Beth-lehem and it was when came they Beth-lehem and it was excited all the city on them and they [fem] said ¿ [is] this Naomi.
20 Akawaambia, “Msiniite tena Naomi, niiteni Mara, kwa sababu Mwenyezi amenitendea mambo machungu sana.
And she said to them may not you call me Naomi call me Mara for he has caused bitterness [the] Almighty to me exceedingly.
21 Mimi niliondoka hali nimejaa, lakini Bwana amenirudisha mtupu. Kwa nini kuniita Naomi? Bwana amenitendea mambo machungu; Mwenyezi ameniletea msiba.”
I full I went and empty he has brought back me Yahweh why? do you call me Naomi and Yahweh he has testified against me and [the] Almighty he has done harm to me.
22 Kwa hiyo Naomi alirudi pamoja na Ruthu Mmoabu mkwe wake, nao wakafika Bethlehemu mwanzoni mwa kuvuna shayiri.
And she returned Naomi and Ruth the Moabite [woman] daughter-in-law her [was] with her who returned from [the] region of Moab and they they came Beth-lehem at [the] beginning of [the] harvest of barley.

< Ruth 1 >