< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
بوعز به دروازهٔ شهر که محل اجتماع مردم شهر بود رفت و در آنجا نشست. آنگاه آن مرد که نزدیکترین خویشاوند شوهر نعومی بود به آنجا آمد. بوعز او را صدا زده گفت: «بیا اینجا! می‌خواهم چند کلمه‌ای با تو صحبت کنم.» او آمد و نزد بوعز نشست.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
آنگاه بوعز ده نفر از ریش‌سفیدان شهر را دعوت کرد تا شاهد باشند.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
بوعز به خویشاوند خود گفت: «تو می‌دانی که نعومی از سرزمین موآب برگشته است. او در نظر دارد ملک برادرمان الیملک را بفروشد.
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
فکر کردم بهتر است در این باره با تو صحبت کنم تا اگر مایل باشی، در حضور این جمع آن را خریداری نمایی. اگر خریدار آن هستی همین حالا بگو. در غیر این صورت خودم آن را می‌خرم. اما تو بر من مقدم هستی و بعد از تو حق من است که آن ملک را خریداری نمایم.» آن مرد جواب داد: «بسیار خوب، من آن را می‌خرم.»
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
بوعز به او گفت: «تو که زمین را می‌خری موظف هستی با روت نیز ازدواج کنی تا بچه‌دار شود و فرزندانش وارث آن زمین گردند و به این وسیله نام شوهرش زنده بماند.»
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
آن مرد گفت: «در این صورت من از حق خرید زمین می‌گذرم، زیرا فرزند روت وارث ملک من نیز خواهد بود. تو آن را خریداری کن.»
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
(در آن روزگار در اسرائیل مرسوم بود که هرگاه شخصی می‌خواست حق خرید ملکی را به دیگری واگذار کند، کفشش را از پا درمی‌آورد و به او می‌داد. این عمل، معامله را در نظر مردم معتبر می‌ساخت.)
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
پس آن مرد وقتی به بوعز گفت: «تو آن زمین را خریداری کن»، کفشش را از پا درآورد و به او داد.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
آنگاه بوعز به ریش‌سفیدان محل و مردمی که در آنجا ایستاده بودند گفت: «شما شاهد باشید که امروز من تمام املاک الیملک، کلیون و محلون را از نعومی خریدم.
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
در ضمن با روت موآبی، زن بیوهٔ محلون ازدواج خواهم کرد تا او پسری بیاورد که وارث شوهر مرحومش گردد و به این وسیله نام او در خاندان و در زادگاهش زنده بماند.»
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
همهٔ مشایخ و مردمی که در آنجا بودند گفتند: «ما شاهد بر این معامله هستیم. خداوند این زنی را که به خانهٔ تو خواهد آمد، مانند راحیل و لیه بسازد که با هم دودمان اسرائیل را بنا کردند. باشد که تو در افراته و بیت‌لحم معروف و کامیاب شوی.
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
با فرزندانی که خداوند به وسیلۀ این زن به تو می‌بخشد، خاندان تو مانند خاندان فارَص پسر تامار و یهودا باشد.»
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
پس بوعز با روت ازدواج کرد و خداوند به آنها پسری بخشید.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
زنان شهر بیت‌لحم به نعومی گفتند: «سپاس بر خداوند که تو را بی‌سرپرست نگذاشت و نوه‌ای به تو بخشید. باشد که او در اسرائیل معروف شود.
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
عروست که تو را دوست می‌دارد و برای تو از هفت پسر بهتر بوده، پسری به دنیا آورده است. این پسر جان تو را تازه خواهد کرد و در هنگام پیری از تو مراقبت خواهد نمود.»
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
نعومی نوزاد را در آغوش گرفت و دایهٔ او شد.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
زنان همسایه آن نوزاد را عوبید نامیده گفتند: «پسری برای نعومی متولد شد!» (عوبید پدر یَسا و پدر بزرگ داوود پادشاه است.)
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
این است نسب نامهٔ بوعز که از فارص شروع شده، به داوود ختم می‌شود: فارص، حصرون، رام، عمیناداب، نحشون، سلمون، بوعز، عوبید، یَسا و داوود.
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >