< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
Booz alla vers la porte de la ville, et après s'y être assis, il vit venir le parent dont il avait parlé; et Booz lui dit: Approche, assieds-toi ici, homme dissimulé. Et l'autre approcha et il s'assit.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
Et Booz prit dix des anciens de la ville, et il leur dit: Asseyez-vous là. Et ils s'assirent.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
Et Booz dit au parent le plus proche. Il y a un champ de notre frère Elimélech qui a été donné à Noémi, laquelle est revenue de Moab.
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
Et moi j'ai dit que je t'en informerai et te dirai: Prends-en possession devant ceux qui sont assis, tous anciens de notre peuple. Si tu veut racheter, rachète; si tu ne le veux, déclare-le-moi, je saurai qu'il n'y a plus personne qui doive racheter, et je viens après toi. Et l'autre répondit: Je rachèterai.
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
Et Booz lui dit: Le jour où tu acquerras le champ des mains de Noémi, et du consentement de Ruth la Moabite, femme du défunt, il faudra que tu la prennes aussi afin de faire revivre le nom de son mari sur son héritage.
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
Et le parent le plus proche dit: Je ne suis point capable de le racheter pour moi-même, sinon au détriment de mon propre héritage; rachète pour toi- même ce que j'ai le droit de racheter, parce que je ne puis le racheter.
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
Or, dès longtemps en Israël cette règle existait concernant les rachats, et les marchés: pour confirmer toute parole, l'homme, détachait sa chaussure et la donnait à son proche, qui reprenait son droit de rachat. Tel était le témoignage en Israël.
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
Le parent le plus proche dit donc à Booz: Acquiers pour toi tous, mes droits de rachat. Et il dénoua sa chaussure, et il la lui donna.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
Et Booz dit aux anciens et à tout le peuple: Vous êtes témoins aujourd'hui que j'ai acheté de Noémi tous les biens d'Elimélech et tout ce qui appartenait à Chélaïon et à Maalon
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
Et que de plus, je prends pour ma femme Ruth la Moabite, femme de Maalon, afin de faire revivre le nom du défunt sur son héritage; et le nom du défunt ne sera effacé ni parmi ses frères, ni dans sa tribu. Vous en êtes témoins aujourd'hui.
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
Et tout le peuple qui était près de la porte s'écria: Témoins! Et les anciens dirent: Fasse le Seigneur que la femme qui entre dans ta maison soit comme Rachel et comme Lia, qui l'une et l'autre ont fondé la maison d'Israël, et ont été des femmes fortes en Ephratha; que son nom demeure en Bethléem.
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
Et que ta maison ressemble à la maison de Pharès que Thamar enfanta à Juda, par la postérité que le Seigneur fera naître pour toi de cette jeune servante.
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
Booz prit donc Ruth pour sa femme et il eut commerce avec elle; le Seigneur lui accorda de concevoir, et elle enfanta un fils.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
Et les femmes dirent à Noémi: Béni soit le Seigneur qui ne t'a point laissé manquer d'un rédempteur, et qui veut aujourd'hui que ton nom vive en Israël.
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
Tu auras un soutien qui ranimera ton âme, qui nourrira ta vieillesse: ta belle-fille qui t'aime, et qui vaut mieux pour toi que sept fils, l'a enfanté.
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
Et Noémi prit l'enfant et elle le mit dans son sein, et elle fut pour Iui comme une nourrice.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
Et les voisins lui donnèrent un nom, disant: Un fils est né à Noémi, et ils le nommèrent Obed; c'est lui qui fut le père de Jessé, père de David.
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
Et voici la postérité de Pharès: Pharès engendra Esron;
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
Et Esron engendra Aram, et Aram engendra Aminadab;
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
Et Aminadab engendra Naasson, et Naasson engendra Salmon;
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
Et Salmon engendra Booz, et Booz engendra Obed;
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
Et Obed engendra Jessé, et Jessé engendra David.

< Ruth 4 >