< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
Or Boaz monta à la porte et s'y assit. Et voici qu'arrive le proche parent dont Boaz avait parlé. Boaz lui dit: « Viens ici, mon ami, et assieds-toi. » Il s'approcha et s'assit.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
Boaz prit dix hommes parmi les anciens de la ville, et dit: « Assieds-toi ici. » Et ils s'assirent.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
Il dit au parent le plus proche: « Naomi, qui est revenue du pays de Moab, vend la parcelle de terre qui appartenait à notre frère Elimelech.
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
J'ai pensé que je devais te le dire, en disant: « Achète-le devant ceux qui sont assis ici, et devant les anciens de mon peuple. Si tu veux la racheter, rachète-la; mais si tu ne veux pas la racheter, dis-le moi, pour que je le sache. Car il n'y a personne d'autre que toi pour la racheter, et je suis après toi. » Il a dit: « Je vais la racheter. »
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
Et Boaz dit: « Le jour où tu achèteras le champ de la main de Naomi, tu devras l'acheter aussi de Ruth la Moabite, la femme du mort, pour relever le nom du mort sur son héritage. »
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
Le proche parent dit: « Je ne peux pas le racheter pour moi-même, de peur de mettre en danger mon propre héritage. Prends pour toi mon droit de rachat, car je ne peux pas le racheter. »
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
Or voici comment on procédait autrefois en Israël pour racheter et pour échanger, afin de confirmer toutes choses: un homme ôtait sa sandale et la donnait à son prochain; et c'était ainsi qu'on officialisait les transactions en Israël.
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
Le proche parent dit à Boaz: « Achète-le pour toi », et il ôta sa sandale.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
Boaz dit aux anciens et à tout le peuple: « Vous êtes témoins aujourd'hui que j'ai acheté de la main de Naomi tout ce qui appartenait à Elimélek, à Chilion et à Mahlon.
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
De plus, j'ai acheté Ruth la Moabite, femme de Mahlon, pour en faire ma femme, afin de relever le nom du défunt sur son héritage, pour que le nom du défunt ne soit pas retranché du milieu de ses frères et de la porte de son lieu. Vous êtes aujourd'hui témoins. »
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
Tout le peuple qui était à la porte, et les anciens, dirent: « Nous sommes témoins. Que l'Éternel rende la femme qui est entrée dans ta maison semblable à Rachel et à Léa, qui toutes deux ont bâti la maison d'Israël; qu'il te traite dignement à Éphrata, et qu'il soit célèbre à Bethléem.
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
Que ta maison soit semblable à la maison de Pérez, que Tamar a enfanté à Juda, de la descendance que Yahvé te donnera par cette jeune femme. »
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
Et Boaz prit Ruth, et elle devint sa femme; il alla vers elle, et Yahvé lui permit de concevoir, et elle enfanta un fils.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
Les femmes dirent à Naomi: « Béni soit Yahvé, qui ne t'a pas laissé aujourd'hui sans parent proche. Que son nom soit célèbre en Israël.
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
Il te rendra la vie et te soutiendra dans ta vieillesse, car ta belle-fille, qui t'aime et qui vaut mieux pour toi que sept fils, lui a donné naissance. »
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
Naomi prit l'enfant, le coucha dans son sein et en prit soin.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
Les femmes, ses voisines, lui donnèrent un nom, en disant: « Un fils est né à Naomi ». Elles lui donnèrent le nom d'Obed. Il est le père de Jessé, le père de David.
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
Et voici l'histoire des générations de Pérez: Pérez engendra Hetsron,
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
et Hetsron engendra Ram, et Ram engendra Amminadab,
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
et Amminadab engendra Nahshon, et Nahshon engendra Salmon,
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
et Salmon engendra Boaz, et Boaz engendra Obed,
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
et Obed engendra Isaï, et Isaï engendra David.

< Ruth 4 >