< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
and Boaz to ascend: rise [the] gate and to dwell there and behold [the] to redeem: redeem to pass which to speak: speak Boaz and to say to turn aside: turn aside [emph?] to dwell [emph?] here someone someone and to turn aside: turn aside and to dwell
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
and to take: take ten human from old: elder [the] city and to say to dwell here and to dwell
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
and to say to/for to redeem: redeem portion [the] land: country which to/for brother: male-relative our to/for Elimelech to sell Naomi [the] to return: return from land: country Moab
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
and I to say to reveal: reveal ear: to ears your to/for to say to buy before [the] to dwell and before old: elder people my if to redeem: redeem to redeem: redeem and if not to redeem: redeem to tell [emph?] to/for me (and to know *Q(K)*) for nothing exception you to/for to redeem: redeem and I after you and to say I to redeem: redeem
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
and to say Boaz in/on/with day to buy you [the] land: country from hand Naomi and from with Ruth [the] Moabite woman: wife [the] to die (to buy *Q(K)*) to/for to arise: establish name [the] to die upon inheritance his
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
and to say [the] to redeem: redeem not be able (to/for to redeem: redeem *Q(k)*) to/for me lest to ruin [obj] inheritance my to redeem: redeem to/for you you(m. s.) [obj] redemption my for not be able to/for to redeem: redeem
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
and this to/for face: before in/on/with Israel upon [the] redemption and upon [the] exchange to/for to arise: establish all word: case to draw man: anyone sandal his and to give: give to/for neighbor his and this [the] testimony in/on/with Israel
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
and to say [the] to redeem: redeem to/for Boaz to buy to/for you and to draw sandal his
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
and to say Boaz to/for old: elder and all [the] people witness you(m. p.) [the] day: today for to buy [obj] all which to/for Elimelech and [obj] all which to/for Chilion and Mahlon from hand Naomi
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
and also [obj] Ruth [the] Moabite woman: wife Mahlon to buy to/for me to/for woman: wife to/for to arise: establish name [the] to die upon inheritance his and not to cut: eliminate name [the] to die from from with brother: male-relative his and from gate place his witness you(m. p.) [the] day: today
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
and to say all [the] people which in/on/with gate and [the] old: elder witness to give: make LORD [obj] [the] woman [the] to come (in): come to(wards) house: household your like/as Rachel and like/as Leah which to build two their [obj] house: household Israel and to make: do strength: worthy in/on/with Ephrath and to call: call by name in/on/with Bethlehem Bethlehem
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
and to be house: household your like/as house: household Perez which to beget Tamar to/for Judah from [the] seed: children which to give: give LORD to/for you from [the] maiden [the] this
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
and to take: take Boaz [obj] Ruth and to be to/for him to/for woman: wife and to come (in): come to(wards) her and to give: give LORD to/for her conception and to beget son: child
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
and to say [the] woman to(wards) Naomi to bless LORD which not to cease to/for you to redeem: redeem [the] day: today and to call: call by name his in/on/with Israel
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
and to be to/for you to/for to return: rescue soul: life and to/for to sustain [obj] greyheaded your for daughter-in-law your which to love: lover you to beget him which he/she/it pleasant to/for you from seven son: child
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
and to take: take Naomi [obj] [the] youth and to set: put him in/on/with bosom: embrace her and to be to/for him to/for be faithful
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
and to call: call by to/for him [the] neighboring name to/for to say to beget son: child to/for Naomi and to call: call by name his Obed he/she/it father Jesse father David
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
and these generation Perez Perez to beget [obj] Hezron
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
and Hezron to beget [obj] Ram and Ram to beget [obj] Amminadab
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
and Amminadab to beget [obj] Nahshon and Nahshon to beget [obj] Salmon
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
and Salmon to beget [obj] Boaz and Boaz to beget [obj] Obed
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
and Obed to beget [obj] Jesse and Jesse to beget [obj] David

< Ruth 4 >