< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
Now, Boaz, went up to the gate, and sat him down there, and lo! the kinsman, passing by, of whom Boaz had spoken, so he said—Turn aside! and sit down here, such a one! And he turned aside, and sat down.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
Then fetched he ten men of the elders of the city, and said—Sit ye down here. And they sat down.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
Then said he to the kinsman, The parcel of land that was our brother Elimelech’s, is to be disposed of by Naomi, who hath returned out of the country of Moab;
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
and, I, thought, I would unveil thine ear, saying—Take it over in presence of such as are here seated, and in presence of the elders of my people. If thou wilt act as kinsman, act as kinsman, but, if thou wilt not so act, only tell me—that I may know, for there is none who can set thee aside as kinsman, but, I, am after thee. And he said, I, will act as kinsman.
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
Then said Boaz, What day thou takest over the land from the hand of Naomi, also, of Ruth the Moabitess, wife of the dead, dost thou take [it], to raise up the name of the dead upon his inheritance.
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
Then said the kinsman—I cannot act as kinsman for myself, lest I mar my own inheritance, —do, thou, for thyself act as kinsman in my right, for I cannot so redeem.
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
Now, this aforetime, [was the way] in Israel, at a redeeming, and at an exchanging, to confirm every word: A man drew off his shoe, and gave it to his neighbour, —yea, this, was the way of taking to witness, in Israel.
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
So the kinsman said unto Boaz, Take it over for thyself, —and he drew off his shoe.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
Then said Boaz to the elders, and all the people—Witnesses, are ye to-day, that I have taken over all that was Elimelech’s, and all that was Chilion’s, and Mahlon’s, —from the hand of Naomi:
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
Moreover, Ruth the Moabitess, wife of Mahlon, have I taken over, to be my wife, to raise up the name of the dead upon his inheritance, that the name of the dead be not cut off—from among his brethren, and from the gate of his dwelling- place, —Witnesses, are ye to-day!
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
Then said all the people who were in the gate, and the elders—Witnesses!, —Yahweh grant the woman who is coming into thy house, to be as Rachel, and as Leah, which two of them did build the house of Israel. Do thou bravely, then, in Ephrathah, and proclaim thou a name in Bethlehem,
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
And let thy house be like the house of Perez, whom Tamar bare to Judah, —of the seed which—may Yahweh give thee, of this young woman.
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
So Boaz took Ruth, and she became his wife, and he went in unto her, —and Yahweh granted her conception, and she bare a son.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
Then said the women unto Naomi, Blessed, be Yahweh! who hath not let thee fail of a kinsman to-day, —and may his name, be proclaimed, in Israel;
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
So shall he become a restorer of thy life, and a nourisher of thine old age, —for, thy daughter-in-law who loveth thee, hath borne him, even, she, who is better to thee than seven sons.
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
So Naomi took the boy, and laid him in her bosom, and she became his nurse.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
And the women, her neighbours, gave him a name, saying, There is born a son to Naomi, —So they called his name Obed, he, was, the father of Jesse, the father of David.
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
These, then, are the generations of Perez: Perez, begat, Hezron;
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
And, Hezron, begat, Ram, and, Ram, begat, Amminadab;
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
And, Amminadab, begat Nahshon, and, Nahshon, begat, Salmon,
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
And, Salmon, begat, Boaz, and, Boaz, begat, Obed;
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
And, Obed, begat, Jesse, and, Jesse, begat, David.

< Ruth 4 >