< Ruth 4 >
1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
Tedy Bóz všed do brány, posadil se tam. A aj, příbuzný ten, o němž on byl mluvil, šel tudy. I řekl jemu: Poď sem, a poseď tuto. Kterýž zastaviv se, sedl.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
A vzav Bóz deset mužů z starších města toho, řekl: Posaďte se tuto. I posadili se.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
Tedy řekl příbuznému tomu: Díl pole, kteréž bylo bratra našeho Elimelecha, prodala Noémi, kteráž se navrátila z krajiny Moábské.
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
A já jsem umínil netajiti toho před tebou, a pravímť: Ujmi pole to před přísedícími těmito a staršími lidu mého. Jestliže chceš koupiti, kup; pakli nekoupíš, oznam mi. Nebo vím, že kromě tebe není žádného, kterýž by měl právo koupiti je, a já jsem po tobě. Tedy on řekl: Já koupím.
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
I řekl Bóz: Když ujmeš pole to od Noémi, tedy i Rut Moábskou, manželku mrtvého, sobě pojmeš, abys vzbudil jméno mrtvého v dědictví jeho.
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
Odpověděl příbuzný ten: Nemohuť koupiti, abych snad nezahladil dědictví svého. Uživ ty práva příbuznosti mé, nebo já ho nemohu užiti.
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
(Byl pak ten obyčej od starodávna v Izraeli při koupi a směnách, ku potvrzení všelijakého jednání, že szul jeden obuv svou, a dal ji druhému. A to bylo na svědectví té věci v Izraeli.)
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
Protož řekl příbuzný Bózovi: Ujmi ty. I szul obuv svou.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
Tedy řekl Bóz starším těm a všemu lidu: Vy svědkové jste dnes, že jsem ujal všecko, což bylo Elimelechovo, i všecko to, což bylo Chelionovo a Mahalonovo, od Noémi.
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
Ano i Rut Moábskou, ženu Mahalonovu, vzal jsem sobě za manželku, abych vzbudil jméno mrtvého v dědictví jeho, a aby nebylo zahlazeno jméno mrtvého z bratří jeho, a z brány místa jeho. Vy svědkové jste dnes toho.
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
I řekl všecken lid, kterýž byl v bráně města, i starší: Svědkové jsme. Dejž Hospodin, aby žena vcházející do domu tvého byla jako Ráchel a jako Lía, kteréžto dvě vzdělaly dům Izraelský. Počínejž sobě zmužile v Efratě, a dosáhni jména v Betlémě.
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
A ať jest dům tvůj jako dům Fáresa, (kteréhož porodila Támar Judovi, ) z semene toho, kteréž by dal tobě Hospodin s mladicí touto.
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
A tak Bóz pojal sobě Rut, a byla manželkou jeho. A když všel k ní, dal jí to Hospodin, že počala a porodila syna.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
I řekly ženy Noémi: Požehnaný Hospodin, kterýž nedopustil toho, abys měla zbavena býti příbuzného v tento čas, tak aby trvalo v Izraeli jméno jeho.
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
Onť očerství duši tvou, a chovati tě bude v starosti tvé; nebo nevěsta tvá, kteráž tě miluje, porodila ho, kteráž tobě lepší jest, nežli sedm synů.
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
Tedy vzavši Noémi dítě, položila je na klín svůj, a byla pěstounkou jeho.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
Daly mu pak jméno sousedy, kteréž pravily: Narodil se syn Noémi, a nazvaly ho jménem Obéd. Onť jest otec Izai, otce Davidova.
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
A tito jsou rodové Fáresovi: Fáres zplodil Ezrona;
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
Ezron pak zplodil Rama, Ram pak zplodil Aminadaba;
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
Aminadab pak zplodil Názona, Názon pak zplodil Salmona;
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
Salmon pak zplodil Bóza, Bóz pak zplodil Obéda;
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
Obéd pak zplodil Izai, Izai pak zplodil Davida.