< Ruth 4 >

1 Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
И Вооз възлезе на портата и седна там; и, ето, минаваше близкият сродник, за когото беше говорил Вооз. И рече: Господине, свърни, седни тук. И той свърна и седна.
2 Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
Тогава Вооз събра десет мъже от градските старейшини и рече: Седнете тук. И те седнаха.
3 Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
После рече на сродника: Ноемин, която се върна от Моавската земя, продава нивата, дяла, който принадлежеше на брата ни Елимелеха;
4 Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
а аз рекох да ти известя и да ти кажа: Купи го пред седящите тука, пред старейшините на людете ми. Ако щеш да го откупиш като сродник, откупи го; но, ако не щеш да го откупиш, кажи ми, за да зная; защото освен тебе, няма друг да го откупи, като сродник; и аз съм подир тебе. И той рече: Аз ще го откупя.
5 Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
И рече Вооз: В деня, когато купиш нивата от ръката на Ноемин, трябва да я купиш и от моавката Рут, жена на умрелия, за да възстановиш името на умрелия над наследството му.
6 Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
Тогава сродникът рече: Не мога да изпълня длъжността на сродник, да не би да напакостя на своето си наследство; ти приеми върху себе си моето право да откупя, защото не мога да откупя нивата.
7 (Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
А в старо време, за да се утвърди всяко дело по откупване и размяна в Израиля, ето що беше обичаят: човекът изуваше обувката си, та я даваше на ближния си: и така се свидетелствуваше в Израиля.
8 Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
За това, сродникът като каза на Вооза: Купи го ти за себе си, изу си обувката.
9 Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
Тогава Вооз каза на старейшините и на всичките люде: Днес сте свидетели, че купувам от ръката на Ноемин всичко, що беше Елимелехово и всичко що беше Хелеоново и Маалоново.
10 Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
А още и моавката Рут Маалоновата жена, придобих за жена, за да възстановя името на умрелия над наследството му, за да се не изличи името на умрелия измежду братята му и из града на обитаването му; вие сте свидетели днес.
11 Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
И всичките люде, които бяха в портата, и старейшините рекоха: Свидетели сме. Господ да направи жената, която влиза в дома ти, като Рахил и като Лия, двете, които са съградили Израилевия дом; и да станеш силен в Ефрата, и да бъдеш знаменит във Витлеем;
12 Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
и от потомството, което Господ ще ти даде от тая млада жена, нека бъде домът ти като дома на Фареса, когото Тамар роди на Юда.
13 Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
И така, Вооз взе Рут, и тя му стана жена; и като влезе при нея, Господ й даде зачатие, и тя роди син.
14 Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
И жените казаха на Ноемин: Благословен Господ, Който днес не те остави без сродник; нека бъде прочуто Името Му в Израиля.
15 Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
Тоя син ще ти бъде обнова на живота и прехрана в старините ти; защото го роди снаха ти, която те обича, която е за тебе по-желателна от седем сина.
16 Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
И Ноемин взе детето и тури го в пазухата си, и стана му кърмилница.
17 Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
И съседките ме дадоха име казвайки: Син се роди на Ноемин. И рекоха го Овид; той е баща на Есея, Давидовия баща.
18 Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
И ето Фаресовото родословие: Фарес роди Есрона,
19 Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
Есрон роди Арама, Арам роди Аминадава,
20 Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
Аминадав роди Наасона, Наасон роди Салмона,
21 Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
Салмон роди Вооза, Вооз роди Овида,
22 Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.
Овид роди Есея, а Есей роди Давида.

< Ruth 4 >