< Ruth 2 >

1 Basi Naomi alikuwa na jamaa wa upande wa mume wake, kutoka ukoo wa Elimeleki, mtu maarufu ambaye aliitwa Boazi.
And [belonged] to Naomi (a relative *Q(K)*) of husband her a man mighty of wealth from [the] clan of Elimelech and name his [was] Boaz.
2 Ruthu, Mmoabu, akamwambia Naomi, “Nitakwenda mashambani nikaokote mabaki ya nafaka nyuma ya yule nitakayepata kibali machoni pake.” Naomi akamwambia, “Nenda, binti yangu.”
And she said Ruth the Moabite [woman] to Naomi let me go please the field (so I may glean *L(ah+b)*) (among the ears of grain *L(abh)*) behind [the one] whom I will find favor in view his and she said to her go O daughter my.
3 Basi akaenda, akaokota mabaki ya nafaka mashambani nyuma ya wavunaji. Ikatokea kwamba alijikuta anafanya kazi kwenye shamba lililokuwa mali ya Boazi, ambaye alitoka kwenye ukoo wa Elimeleki.
And she went and she came and she gleaned in the field behind the harvesters and it chanced on chance her [the] portion of the field of Boaz who [was] from [the] clan of Elimelech.
4 Papo hapo Boazi akarudi kutoka Bethlehemu, akawasalimu wavunaji, akasema, “Bwana awe nanyi!” Nao wakamjibu, “Bwana akubariki.”
And there! Boaz [was] coming from Beth-lehem and he said to the harvesters Yahweh [be] with you and they said to him may he bless you Yahweh.
5 Boazi akamuuliza msimamizi wa wavunaji, “Je, yule mwanamwali ni wa nani?”
And he said Boaz to servant his who was appointed over the harvesters [belongs] to whom? the young woman this.
6 Msimamizi akamjibu, “Ni yule Mmoabu aliyerudi kutoka nchi ya Moabu pamoja na Naomi.
And he answered the servant who was appointed over the harvesters and he said [is] a young woman Moabite she who returned with Naomi from [the] region of Moab.
7 Yeye aliomba, ‘Tafadhali niruhusu niokote na kukusanya miongoni mwa miganda nyuma ya wavunaji.’ Naye ameshinda shambani tangu asubuhi pasipo kupumzika, isipokuwa kwa muda mfupi kivulini.”
And she said let me glean please and I will gather among the sheaves behind the harvesters and she came and she has stayed from then this morning and until now this sitting she the house little.
8 Kisha Boazi akamwambia Ruthu, “Binti yangu, nisikilize. Usiende kuokota mabaki ya mavuno katika shamba lingine, na usiondoke hapa. Kaa hapa na hawa watumishi wangu wa kike.
And he said Boaz to Ruth ¿ not have you heard O daughter my may not you go to glean in a field another and also not you must pass on from this [field] and thus you will stay! with female servants my.
9 Angalia shamba wanaume wanamovuna, ufuate nyuma yao. Nimewaamuru wanaume hawa wasikuguse. Wakati wowote ukiona kiu, nenda kwenye mitungi ukanywe maji waliyoyateka wanaume hawa.”
Eyes your [be] on the field which they are harvesting! (and you will go *L(abh)*) behind them ¿ not have I commanded the young men to not to touch you and you will be thirsty and you will go to the vessels and you will drink some of [that] which they will draw! the young men.
10 Kwa ajili ya hili, akasujudu mpaka nchi, akamwambia, “Jinsi gani nimepata kibali machoni pako, hata ukanijali mimi mgeni?”
And she fell on face her and she bowed down [the] ground towards and she said to him why? have I found favor in view your to pay regard to me (and I *L(abh)*) [am] a foreigner.
11 Boazi akamjibu, “Nimeambiwa yote uliyomtendea mama mkwe wako tangu mume wako alipofariki, na jinsi ulivyomwacha baba yako na mama yako na nchi yako ulimozaliwa, ukaja kuishi na watu ambao hukuwafahamu awali.
And he answered Boaz and he said to her certainly it has been told to me all that you have done with mother-in-law your after [the] death of husband your and you left (father your *L(abh)*) and mother your and [the] land of kindred your and you came to a people which not you knew yesterday three days ago.
12 Bwana na akulipe kwa yale uliyoyatenda. Ubarikiwe kwa wingi na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekimbilia mabawani mwake.”
May he reward Yahweh deed[s] your and may it be wage[s] your complete from with Yahweh [the] God of Israel whom you have come to take refuge under wings his.
13 Kisha Ruthu akasema, “Naomba niendelee kupata kibali machoni pako, bwana wangu. Kwa maana umenifariji na umezungumza kwa ukarimu na mjakazi wako, hata ingawa mimi si bora kama mmoja wa watumishi wako wa kike.”
And she said I am finding favor in view your O lord my for you have comforted me and for you have spoken to [the] heart of maidservant your and I not I am like one of maidservants your.
14 Wakati wa chakula, Boazi akamwambia Ruthu, “Karibia hapa. Kula mkate na uchovye ndani ya siki.” Alipoketi pamoja na wavunaji, akampa nafaka zilizookwa. Akala kiasi alichotaka na kusaza.
And he said to her Boaz to [the] time of the meal approach here and you will eat some of the food and you will dip portion your in the vinegar and she sat down from [the] side of the harvesters and he held out to her roasted grain and she ate and she was satisfied and she had excess.
15 Alipoinuka ili kuokota mabaki ya nafaka, Boazi akawaagiza watu wake, “Hata kama atakusanya kati ya miganda, msimzuie.
And she arose to glean and he commanded Boaz servants his saying also between the sheaves she will glean and not you must humiliate her.
16 Badala yake, toeni masuke katika miganda, mwachieni ayaokote, na msimkemee.”
And also indeed you will pull out for her some of the bundles of grain and you will leave [them] and she will glean and not you must rebuke her.
17 Basi Ruthu akaokota masazo shambani hata jioni. Akatwanga ile shayiri aliyokusanya, ikajaa efa moja.
And she gleaned in the field until the evening and she beat out [that] which she had gleaned and it was about an ephah barley.
18 Akaibeba na kuelekea mjini, naye mama mkwe wake akaona jinsi alivyoweza kuokota nafaka nyingi. Pia Ruthu akachukua kile alichobakiza baada ya kula na kushiba, akampa.
And she lifted [it] up and she went the city and she saw mother-in-law her [that] which she had gleaned and she took [it] out and she gave to her [that] which she had left over from abundance her.
19 Basi mkwewe akamuuliza, “Je, umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Abarikiwe mtu yule aliyekujali.” Ndipo Ruthu akamwambia mama mkwe wake juu ya yule ambaye yeye alikuwa amefanyia kazi katika shamba lake. Akasema, “Yule mtu niliyefanyia kazi kwake leo, anaitwa Boazi.”
And she said to her mother-in-law her where? did you glean this day and where? did you work may he be [the one who] paid regard to you blessed and she told to mother-in-law her whom she had worked with him and she said [the] name of the man whom I worked with him this day [is] Boaz.
20 Naye Naomi akamwambia mkwewe, “Bwana ambariki! Hakuacha kuonyesha fadhili zake kwa walio hai na kwa waliokufa.” Pia akamwambia, “Huyo mtu ni mmoja wa jamaa yetu wa karibu anayestahili kutukomboa.”
And she said Naomi to daughter-in-law her [be] blessed he by Yahweh who not he has forsaken covenant loyalty his with the living and with the dead and she said to her Naomi [is] near to us the man [is] one of kinsman-redeemer[s] our he.
21 Kisha Ruthu, Mmoabu, akasema, “Hata aliniambia, ‘Kaa pamoja na watumishi wangu mpaka watakapomaliza kuvuna nafaka yangu yote.’”
And she said Ruth the Moabite [woman] also - that he said to me with the servants who [belong] to me you will stay! until they have completed all the harvest which [belongs] to me.
22 Kisha Naomi akamwambia Ruthu mkwewe, “Binti yangu, itakuwa vyema wewe ufuatane na wasichana wake, kwa sababu katika shamba la mtu mwingine wanaweza kukudhuru.”
And she said Naomi to Ruth daughter-in-law her [is] good O daughter my that you will go out with female servants his and not people will molest you in a field another.
23 Kwa hivyo Ruthu akafuatana na watumishi wa kike wa Boazi, akaokota mpaka mwisho wa mavuno ya shayiri na ya ngano. Naye aliishi na mama mkwe wake.
And she stayed with [the] female servants of Boaz to glean until was complete [the] harvest of the barley and [the] harvest of the wheat and she dwelt with mother-in-law her.

< Ruth 2 >