< Ruth 1 >

1 Wakati Waamuzi walipotawala Israeli, kulikuwa na njaa katika nchi. Mtu mmoja kutoka nchi ya Bethlehemu ya Yuda, pamoja na mke wake na wanawe wawili, akaenda kuishi katika nchi ya Moabu.
AND IT came to pass in the days when the judges judged, that there was a famine in the land. And a certain man of Beth-lehem in Judah went to sojourn in the field of Moab, he, and his wife, and his two sons.
2 Mtu huyu aliitwa Elimeleki, mkewe aliitwa Naomi, na hao wanawe wawili waliitwa Maloni na Kilioni. Walikuwa Waefrathi kutoka Bethlehemu ya Yuda. Wakaenda katika nchi ya Moabu, wakaishi huko.
And the name of the man was Elimelech, and the name of his wife Naomi, and the name of his two sons Mahlon and Chilion, Ephrathites of Beth-lehem in Judah. And they came into the field of Moab, and continued there.
3 Elimeleki mumewe Naomi akafa, hivyo Naomi akabaki na wanawe wawili.
And Elimelech Naomi's husband died; and she was left, and her two sons.
4 Nao wakaoa wanawake Wamoabu, jina la mmoja aliitwa Orpa, na wa pili aliitwa Ruthu. Baada ya kama miaka kumi,
And they took them wives of the women of Moab: the name of the one was Orpah, and the name of the other Ruth; and they dwelt there about ten years.
5 Maloni na Kilioni pia wakafa. Basi Naomi akabaki hana mume wala wanawe wawili.
And Mahlon and Chilion died both of them; and the woman was left of her two children and of her husband.
6 Aliposikia akiwa huko Moabu kwamba Bwana amewasaidia watu wake kwa kuwapa chakula, Naomi na wakweze wakajiandaa kurudi nyumbani.
Then she arose with her daughters-in-law, that she might return from the field of Moab; for she had heard in the field of Moab how that the LORD had remembered His people in giving them bread.
7 Yeye na wakweze wawili wakaondoka pale walipokuwa wakiishi na kushika njia kurudi nchi ya Yuda.
And she went forth out of the place where she was, and her two daughters-in-law with her; and they went on the way to return unto the land of Judah.
8 Ndipo Naomi akawaambia wale wakwe zake wawili, “Rudini, kila mmoja wenu nyumbani kwa mama yake. Bwana na awatendee fadhili kama mlivyowatendea hao waliofariki, na pia mimi.
And Naomi said unto her two daughters-in-law: 'Go, return each of you to her mother's house; the LORD deal kindly with you, as ye have dealt with the dead, and with me.
9 Bwana na amjalie kila mmoja wenu maisha mema nyumbani kwa mume mwingine.” Kisha akawabusu, nao wakalia kwa sauti kubwa,
The LORD grant you that ye may find rest, each of you in the house of her husband.' Then she kissed them; and they lifted up their voice, and wept.
10 wakamwambia, “Tutarudi pamoja na wewe nyumbani kwa watu wako.”
And they said unto her: 'Nay, but we will return with thee unto thy people.'
11 Lakini Naomi akasema, “Rudini nyumbani, binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, mimi nitaweza tena kuwa na wana wengine ambao wataweza kuwaoa ninyi?
And Naomi said: 'Turn back, my daughters; why will ye go with me? have I yet sons in my womb, that they may be your husbands?
12 Rudini nyumbani, binti zangu; mimi ni mzee kiasi kwamba siwezi kumpata mume mwingine. Hata kama ningefikiria kuwa bado kuna tumaini kwangu, hata kama ningekuwa na mume usiku huu na kuwazaa wana,
Turn back, my daughters, go your way; for I am too old to have a husband. If I should say: I have hope, should I even have an husband to-night, and also bear sons;
13 je, mngesubiri mpaka wakue? Mngebakia bila kuolewa mkiwasubiri? La, hasha, binti zangu. Nimepata uchungu kuliko ninyi, kwa sababu mkono wa Bwana umekuwa kinyume nami!”
would ye tarry for them till they were grown? would ye shut yourselves off for them and have no husbands? nay, my daughters; for it grieveth me much for your sakes, for the hand of the LORD is gone forth against me.'
14 Kisha wakalia tena kwa sauti. Orpa akambusu mama mkwe wake, akaenda zake, lakini Ruthu akaambatana naye.
And they lifted up their voice, and wept again; and Orpah kissed her mother-in-law; but Ruth cleaved unto her.
15 Naomi akamwambia, “Tazama, mwenzako anarejea kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudi pamoja naye.”
And she said: 'Behold, thy sister-in-law is gone back unto her people, and unto her god; return thou after thy sister-in-law.'
16 Lakini Ruthu akajibu, “Usinisihi nikuache au niache kukufuata. Utakakokwenda nami nitakwenda, na wewe utakapoishi nitaishi. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
And Ruth said: 'Entreat me not to leave thee, and to return from following after thee; for whither thou goest, I will go; and where thou lodgest, I will lodge; thy people shall be my people, and thy God my God;
17 Pale utakapofia nami nitafia hapo, na papo hapo nitazikwa. Bwana na aniadhibu vikali, kama kitu kingine chochote kitanitenga nawe isipokuwa kifo.”
where thou diest, will I die, and there will I be buried; the LORD do so to me, and more also, if aught but death part thee and me.'
18 Naomi alipotambua kwamba Ruthu amenuia kufuatana naye, hakuendelea kumsihi tena.
And when she saw that she was stedfastly minded to go with her, she left off speaking unto her.
19 Kwa hiyo hao wanawake wawili wakaondoka, wakafika Bethlehemu. Walipofika Bethlehemu, mji mzima ulitaharuki, wanawake wakashangaa, wakasema, “Huyu aweza kuwa ni Naomi?”
So they two went until they came to Beth-lehem. And it came to pass, when they were come to Beth-lehem, that all the city was astir concerning them, and the women said: 'Is this Naomi?'
20 Akawaambia, “Msiniite tena Naomi, niiteni Mara, kwa sababu Mwenyezi amenitendea mambo machungu sana.
And she said unto them: 'Call me not Naomi, call me Marah; for the Almighty hath dealt very bitterly with me.
21 Mimi niliondoka hali nimejaa, lakini Bwana amenirudisha mtupu. Kwa nini kuniita Naomi? Bwana amenitendea mambo machungu; Mwenyezi ameniletea msiba.”
I went out full, and the LORD hath brought me back home empty; why call ye me Naomi, seeing the LORD hath testified against me, and the Almighty hath afflicted me?'
22 Kwa hiyo Naomi alirudi pamoja na Ruthu Mmoabu mkwe wake, nao wakafika Bethlehemu mwanzoni mwa kuvuna shayiri.
So Naomi returned, and Ruth the Moabitess, her daughter-in-law, with her, who returned out of the field of Moab — and they came to Beth-lehem in the beginning of barley harvest.

< Ruth 1 >