< Warumi 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
Paul renga, Jisua Khrista tîrlâm le tîrton ranga thang, Pathien'n a Thurchi Sa ngei misîr ranga koi.
2 Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
Ma Thurchi Sa hah tien renga Pathien'n a dêipungei mangin a lei khâma, Lekhabu Inthieng taka miziekin.
3 yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
Mahi a Nâipasal, ei Pumapa Jisua Khrista roi ani: Miriem nina tieng chu David richisuonpâra inzir ania;
4 na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
ânthiengna Ratha Inthieng chu, thina renga ânthoinôkna han Pathien Nâipasal ani tie sinthotheina roiinpuitak chu a minlang ani zoi.
5 Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
Ama sika han Pathien'n tîrton ni rangin Khrista jôtna sika sintum ni pêk ani, Ramtina mingei iema le jômna tienga ruoi ngei rangin mikhâm ani.
6 Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
Rom taka om ngei khom nangni huomsa ani, Jisua Khrista ata nirangin nangni a koi ani.
7 Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Masikin Rom taka om Pathien lungkham ngei le ama mi ni ranga a koi ngei nâm ranga ki miziek ani: Pathien ei Pa le Pumapa Jisua Khrista'n, moroina le inngêina nangni pêk rese.
8 Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
Amotontaka, rammuol pumpuia nin taksônna thurchi ânthang sikin nin rênga rangin Jisua Khrista jâra ka Pathien kôm râisânna chong ki mintung bak ani.
9 Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
Chubai ko thona ngeia nangni ki riettit ngâi ti a Nâipasal Thurchi Sa misîra ku mulung murdia sin ko tho ngâi Pathien hah ni rietpuipu ani.
10 katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
A lungdo anînchu atûn luo nangni ko hong sir phâk theina rangin Pathien kôm ke ngên tit ngâi ani.
11 Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
Nin dik nôk uolna rangin ratha satvurna ngei nangni min chang rangin mu rang nangni ku nuom tatak ani.
12 au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
Maha keima le nangni hih nin taksôn han inmohôk inlôm ku nuom ani, ei insan inlôm theina rangin.
13 Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
Ka lâibungngei le sarnungei, nangni hongpan rang ko bôk tit ngâia, hannirese insûkloina a om kelen ngâi ti nin riet ku nuom ani, Jentail dang ngei lâia taksôn thar ka man anghan nin lâia khom man rangin ka sabei.
14 Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
Mitin chunga lâkâi ke nei, Greek mingei le mi môlma ngei mivârngei le mi inmôl ngei kôma khom.
15 Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
Ma anghan nangni Rom khopuia omngei kôma khom Thurchi Sa misîr rangin inthok chakin ko om ani.
16 Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
Thurchisa hih inzakpui mu-ung, tukhom a iem murdi sanminringna ranga Pathien sinthotheina ania, aphuta Judangei ta rangin masuole Jentailngei ta rang khomin ahongni.
17 Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
Thurchisa hin taksôn sik vaia Pathien'n mi thei a minchang lam aphut renga amongna tena a juong minlang ani, Pathien lekhabu'n, “Taksôn sika thei intumpu chu ring a tih,” tia ânziek anghan.
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
Invân renga Pathien taksina hah miriemngei Pathien lunghâng tholoina sietna le dikloina murdi chunga ajuong minlang ani, an sietna sikin chongtak hah an kal tita.
19 kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
Pathien'n intakna a mintuong ngeia, asikchu thurchi rietruongei chu an kôma ânlang tita Pathien'n ama rengin a min riet zoi sikin.
20 Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios )
Anina mita mutheiloi a kumtuong sinthotheina le a Pathien nina hah rammuol sinphut renga a neinun sin ngeia inthârin mutheiin ânlanga. Masikin anni ngei chu jôkna rang lampui ite dôn mak ngei. (aïdios )
21 Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
Pathien an riet chakin Pathien angin chôiminsâng mak ngeia ama kôm râisânchong khom ril mak ngeia; sin kâmboi mang an mindona an mulungrîl sêt tak hah ahong jîng zoia.
22 Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
Avâr okin an inbea hannirese an inmôl ani.
23 na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
Thitheiloi Pathien chubaimûk nêkin a thithei miriemngei le vângei sângei le iring rimilngei pathien an min chang zoia.
24 Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
Masikin, an mulungrîl nuomlam neinun porinchengei tho rangin Pathien'n nûk a song ngeia inzakpui omtakin an om zoi ani.
25 Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn )
Pathien chongtak nêkin milak an thang uola, asinpu biek nêkin a sin ngei biekna sin an thope uola, Asinpu chu kumtuongin minpâkin om rese! Amen. (aiōn )
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
Masika han kêng Pathien'n inzak taka an hur ha phalin nûk a song ngeia. An nupangngei hah khom nunchan insiengpui angtakin om loiin an oma.
27 Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
An pasalngei khom nupang mang ngâi lam mâksanin, hurin an in en inlôma, pasal le pasal dikloi takin an lênga. An taksa ngeia an sietna man an man ani.
28 Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
Pathien rietna diktak hah an mulungrîla an nei nuom loi sikin an mindonna siet tak anga om rangin Pathien'n nûk a song ngeia, an tho loi ruo khom an tho zoia.
29 Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
Dikloina murdi'n an sipa sietnangei, insâp râtnangei, puoloina ngei, narsana ngei, inthatna ngei, insuol inkhalna ngei, inhuongna ngei le inmumâkna ngeiin an sipa,
30 wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
an inêroa, an indema, Pathien an henga, an indoia, an inpâka, an insonga, sietna dadang athar an min suoka, an nulepangei mirit mak ngeia.
31 wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
A sielesarietna nei mak ngeia an inkhâmna mang mak ngeia, midang lungkhamna le inriengmuna reng dôn ngâi mak ngei.
32 Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
Ma anga tho ngei chu Pathien'n a khâm anga thiruo anni ti riet chakin, anni an tho vai niloiin midang a tho ngei khom an nuompui sa ngâi.