< Warumi 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
Paul the seruaut of Iesus Christ called to be an Apostle put a parte to preache the Gospell of God
2 Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
which he promysed afore by his Prophetes in the holy scriptures
3 yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
that make mension of his sonne the which was begotte of the seed of David as pertayninge to the flesshe:
4 na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
and declared to be the sonne of God with power of the holy goost that sanctifieth sence ye tyme that Iesus Christ oure Lorde rose agayne from deeth
5 Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
by whom we have receaved grace and apostleshyppe to bringe all maner hethe people vnto obedience of the fayth that is in his name:
6 Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
of the which hethen are ye a part also which are Iesus christes by vocacio.
7 Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
To all you of Rome beloved of God and saynctes by callinge. Grace be with you and peace from God oure father and from the Lorde Iesus Christ.
8 Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
Fyrst verely I thanke my God thorow Iesus Christ for you all because youre fayth is publisshed through out all the worlde.
9 Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
For God is my witnes whom I serve with my sprete in the Gospell of his sonne that with out ceasinge I make mencion of you alwayes in my prayers
10 katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
besechinge that at one tyme or another a prosperous iorney (by ye will of god) myght fortune me to come vnto you.
11 Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
For I longe to see you that I myght bestowe amoge you some spirituall gyfte to strength you with all:
12 au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
that is that I myght have consolacion together with you through the commen fayth which bothe ye and I have.
13 Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
I wolde that ye shuld knowe brethre how that I have often tymes purposed to come vnto you (but have bene let hitherto) to have some frute amonge you as I have amonge other of ye Gentyls.
14 Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
For I am detter both to the Grekes and to them which are no Grekes vnto the learned and also vnto the vnlearned.
15 Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
Lykewyse as moche as in me is I am redy to preache the Gospell to you of Rome also.
16 Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
For I am not ashamed of the Gospell of Christ because it is ye power of God vnto salvacio to all yt beleve namely to the Iewe and also to ye getyle.
17 Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
For by it ye rightewesnes which cometh of god is opened fro fayth to fayth. As it is written: The iust shall live by fayth.
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
For the wrath of God apereth from heven agaynst all vngodlynes and vnrightewesnes of me which withholde ye trueth in vnrightewesnes
19 kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
seynge what maye be knowen of God that same is manifest amoge them. For God dyd shewe it vnto them.
20 Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios )
So that his invisible thinges: that is to saye his eternall power and godhed are vnderstonde and sene by the workes from the creacion of the worlde. So that they are without excuse (aïdios )
21 Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
in as moche as when they knewe god they glorified him not as God nether were thakfull but wexed full of vanities in their imaginacions and their folisshe hertes were blynded.
22 Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
When they couted them selves wyse they became foles
23 na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
and turned the glory of the immortall god vnto the similitude of the ymage of mortall man and of byrdes and foure foted beastes and of serpentes.
24 Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
Wherfore god lykewyse gave the vp vnto their hertes lustes vnto vnclennes to defyle their awne boddyes bitwene them selves:
25 Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn )
which tourned his truthe vnto a lye and worshipped and served the creatures more then ye maker which is blessed for ever. Ame. (aiōn )
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
For this cause god gave them vp vnto shamfull lustes. For even their wemen did chaunge the naturall vse vnto the vnnaturall.
27 Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
And lyke wyse also the men lefte the naturall vse of the woma and bret in their lustes one on another. And man with man wrought filthynes and receaved in them selves the rewarde of their erroure as it was accordinge.
28 Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
And as it semed not good vnto them to be aknowen of God even so God delivered them vp vnto a leawde mynd yt they shuld do tho thinges which were not comly
29 Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
beinge full of all vnrighteous doinge of fornicacio wickednes coveteousnes maliciousnes full of envie morther debate disseyte evill codicioned whisperers
30 wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
backbyters haters of God doers of wroge proude bosters bringers vp of evyll thinges disobedient to father and mother
31 wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
with out vnderstondinge covenaunte breakers vnlovinge trucebreakers and merciles.
32 Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
Which me though they knew the rightewesnes of God how that they which soche thinges commyt are worthy of deeth yet not only do the same but also have pleasure in them that do them.