< Warumi 9 >

1 Ninasema kweli katika Kristo, wala sisemi uongo, dhamiri yangu inanishuhudia katika Roho Mtakatifu.
Prawdę mówię w Chrystusie, a nie kłamię, w czem mi poświadcza sumienie moje przez Ducha Świętego:
2 Nina huzuni kuu na uchungu usiokoma moyoni mwangu.
Że mam wielki smutek i nieustawający ból w sercu mojem.
3 Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu hasa, wale walio wa kabila langu kwa jinsi ya mwili,
Albowiem żądałbym sam, abym się stał odłączonym od Chrystusa za braci moich, za pokrewnych moich według ciała.
4 yaani, watu wa Israeli, ambao ndio wenye kule kufanywa wana, ule utukufu wa Mungu, yale maagano, kule kupokea sheria, ibada ya kwenye Hekalu na zile ahadi.
Którzy są Izraelczycy, których jest przysposobienie synowskie i chwała, i przymierza, i zakonu danie, i służba Boża, i obietnice;
5 Wao ni wa uzao wa mababa wakuu wa kwanza, ambao kutoka kwao Kristo alikuja kwa jinsi ya mwili kama mwanadamu, yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, mwenye kuhimidiwa milele! Amen. (aiōn g165)
Których są ojcowie i z których poszedł Chrystus ile według ciała, który jest nad wszystkimi Bóg błogosławiony na wieki. Amen. (aiōn g165)
6 Si kwamba Neno la Mungu limeshindwa. Kwa maana si kila Mwisraeli ambaye ni wa uzao utokanao na Israeli ni Mwisraeli halisi.
Lecz nie można, żeby miało upaść słowo Boże; albowiem nie wszyscy, którzy są z Izraela, są Izraelem;
7 Wala hawakuwi wazao wa Abrahamu kwa sababu wao ni watoto wake, lakini: “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.”
Ani iż są nasieniem Abrahamowem, wszyscy są dziećmi; ale rzeczono: W Izaaku będzie tobie nazwane nasienie;
8 Hii ina maana kwamba, si watoto waliozaliwa kimwili walio watoto wa Mungu, bali ni watoto wa ahadi wanaohesabiwa kuwa uzao wa Abrahamu.
To jest, nie dzieci ciała są dziećmi Bożymi; ale dzieci obietnicy bywają w nasienie policzone.
9 Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitakurudia tena wakati kama huu, naye Sara atapata mtoto wa kiume.”
Albowiem obietnicy słowo to jest: O tym właśnie czasie przyjdę, a Sara będzie miała syna;
10 Wala si hivyo tu, bali pia watoto aliowazaa Rebeka walikuwa na baba huyo huyo mmoja, yaani, baba yetu Isaki.
A nie tylko to, ale i Rebeka, gdy z jednego ojca naszego Izaaka brzemienną została.
11 Lakini, hata kabla hao mapacha hawajazaliwa au kufanya jambo lolote jema au baya, ili kwamba kusudi la Mungu la kuchagua lipate kusimama,
Gdy się jeszcze były dziatki nie narodziły, ani co dobrego albo złego uczyniły, aby się ostało postanowienie Boże według wybrania, nie z uczynków, ale z tego, który powołuje,
12 si kwa matendo, bali kwa yeye mwenye kuita, Rebeka aliambiwa, “Yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.”
Rzeczono jej, że większy będzie służył mniejszemu;
13 Kama vile ilivyoandikwa, “Nimempenda Yakobo, lakini nimemchukia Esau.”
Jako napisano: Jakóbam umiłował, alem Ezawa miał w nienawiści.
14 Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha!
Cóż tedy rzeczemy? Jestże niesprawiedliwość u Boga? Nie daj tego Boże!
15 Kwa maana Mungu alimwambia Mose, “Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
Albowiem do Mojżesza mówi: Zmiłuję się, nad kim się zmiłuję; a zlituję się, nad kim się zlituję.
16 Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu.
A przetoż nie zależy na tym co chce, ani na tym, co bieży, ale na Bogu, który się zmiłowywa.
17 Kwa maana Maandiko yamwambia Farao, “Nilikuinua kwa kusudi hili hasa, ili nipate kuonyesha uweza wangu juu yako, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.”
Albowiem mówi Pismo do Faraona: Na tom cię samo wzbudził, abym okazał moc moję na tobie, a iżby opowiadane było imię moje po wszystkiej ziemi.
18 Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia yeye atakaye kumhurumia na humfanya mgumu yeye atakaye kumfanya mgumu.
A tak nad kim chce, zmiłowywa się, a kogo chce, zatwardza.
19 Basi mtaniambia, “Kama ni hivyo, kwa nini basi bado Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kupinga mapenzi yake?”
Ale mi rzeczesz: Przeczże się jeszcze uskarża? bo któż się sprzeciwił woli jego?
20 Lakini, ewe mwanadamu, u nani wewe ushindane na Mungu? “Je, kilichoumbwa chaweza kumwambia yeye aliyekiumba, ‘Kwa nini umeniumba hivi?’”
I owszem, o człowiecze! któżeś ty jest, który spór wiedziesz z Bogiem? Izali lepianka rzecze lepiarzowi: Przeczżeś mię tak uczynił?
21 Je, mfinyanzi hana haki ya kufinyanga kutoka bonge moja vyombo vya udongo, vingine kwa matumizi ya heshima na vingine kwa matumizi ya kawaida?
Izali nie ma mocy garncarz nad gliną, żeby z tejże gliny uczynił jedno naczynie ku uczciwości, a drugie ku zelżywości?
22 Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu?
A jeźliż Bóg chcąc okazać gniew i znajomą uczynić możność swoję, znosił w wielkiej cierpliwości naczynia gniewu na zginienie zgotowane,
23 Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vile vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake,
A iżby znajome uczynił bogactwo chwały swojej nad naczyniem miłosierdzia, które zgotował ku chwale;
24 yaani pamoja na sisi, ambao pia alituita, si kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa?
Których i powołał, to jest nas, nie tylko z Żydów, ale i z poganów.
25 Kama vile Mungu asemavyo katika Hosea: “Nitawaita ‘watu wangu’ wale ambao si watu wangu; nami nitamwita ‘mpenzi wangu’ yeye ambaye si mpenzi wangu,”
Jako też u Ozeasza mówi: Nazwię lud, który nie był moim, ludem moim, a onę, która nie była umiłowaną, nazwię umiłowaną.
26 tena, “Itakuwa hasa mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’”
I stanie się, że na tem miejscu, gdzie im mawiano: Nie jesteście wy ludem moim, tam nazwani będą synami Boga żywego.
27 Isaya anapiga kelele kuhusu Israeli: “Ingawa idadi ya wana wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaookolewa.
A Izajasz woła nad Izraelem, mówiąc: Choćby liczba synów Izraelskich była jako piasek morski, ostatki zachowane będą.
28 Kwa kuwa Bwana ataitekeleza hukumu yake duniani kwa haraka na kwa ukamilifu.”
Albowiem sprawę skończy i skróci w sprawiedliwości; sprawę zaiste skróconą uczyni Pan na ziemi.
29 Ni kama vile alivyotabiri Isaya akisema: “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote asingelituachia uzao, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.”
I jako przedtem powiedział Izajasz: By nam był Pan zastępów nie zostawił nasienia, bylibyśmy się stali jako Sodoma i Gomorze bylibyśmy podobni.
30 Kwa hiyo tuseme nini basi? Kwamba watu wa Mataifa ambao hawakutafuta haki, wamepata haki ile iliyo kwa njia ya imani.
Cóż tedy rzeczemy? To, iż poganie, którzy nie szukali sprawiedliwości, dostąpili sprawiedliwości, a sprawiedliwości, która jest z wiary.
31 Lakini Israeli, ambao walijitahidi kupata haki kwa njia ya sheria, hawakuipata.
A Izrael szukając zakonu sprawiedliwości, nie doszedł zakonu sprawiedliwości.
32 Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa njia ya imani bali kwa njia ya matendo. Wakajikwaa kwenye lile “jiwe la kukwaza.”
Dlaczegoż? Iż nie z wiary, ale jako z uczynków zakonu jej szukali; albowiem się obrazili o kamień obrażenia,
33 Kama ilivyoandikwa: “Tazama naweka katika Sayuni jiwe la kukwaza watu na mwamba wa kuwaangusha. Yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”
Jako napisano: Oto kładę w Syonie kamień obrażenia i opokę otrącenia, a wszelki, który w niego wierzy, nie będzie pohańbiony.

< Warumi 9 >