< Warumi 9 >

1 Ninasema kweli katika Kristo, wala sisemi uongo, dhamiri yangu inanishuhudia katika Roho Mtakatifu.
Stojąc przed obliczem Chrystusa, chcę zgodnie z prawdą i bez kłamstwa, z czystym sumieniem i w Duchu Świętym, powiedzieć,
2 Nina huzuni kuu na uchungu usiokoma moyoni mwangu.
że noszę w sercu głęboki smutek i ból.
3 Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu hasa, wale walio wa kabila langu kwa jinsi ya mwili,
Nawet sam chciałbym być odłączony od Chrystusa, gdyby to pomogło moim rodakom,
4 yaani, watu wa Israeli, ambao ndio wenye kule kufanywa wana, ule utukufu wa Mungu, yale maagano, kule kupokea sheria, ibada ya kwenye Hekalu na zile ahadi.
Izraelitom! To ich właśnie wybrał Bóg, otoczył ich chwałą, zawarł z nimi przymierze, przekazał im Prawo, pokazał, jak mają Mu służyć, i dał tak wiele obietnic.
5 Wao ni wa uzao wa mababa wakuu wa kwanza, ambao kutoka kwao Kristo alikuja kwa jinsi ya mwili kama mwanadamu, yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, mwenye kuhimidiwa milele! Amen. (aiōn g165)
Ich przodkowie kochali Boga i z tego narodu pochodzi Chrystus—Ten, który jest ponad wszystkim, Bóg uwielbiony na wieki. Amen! (aiōn g165)
6 Si kwamba Neno la Mungu limeshindwa. Kwa maana si kila Mwisraeli ambaye ni wa uzao utokanao na Israeli ni Mwisraeli halisi.
Boże obietnice się spełniły. Nie wszyscy bowiem, którzy pochodzą z Izraela, są prawdziwymi Izraelitami.
7 Wala hawakuwi wazao wa Abrahamu kwa sababu wao ni watoto wake, lakini: “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.”
I nie każdy potomek Abrahama jest rzeczywiście jego dzieckiem—Bóg uznał bowiem za jego potomków tylko tych, którzy pochodzą od jego syna Izaaka.
8 Hii ina maana kwamba, si watoto waliozaliwa kimwili walio watoto wa Mungu, bali ni watoto wa ahadi wanaohesabiwa kuwa uzao wa Abrahamu.
Oznacza to, że nie wszystkie dzieci Abrahama są dziećmi Boga, a jedynie te, które urodziły się zgodnie ze złożoną wcześniej Bożą obietnicą.
9 Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitakurudia tena wakati kama huu, naye Sara atapata mtoto wa kiume.”
Brzmiała ona tak: „Za rok o tej porze Sara będzie miała syna”.
10 Wala si hivyo tu, bali pia watoto aliowazaa Rebeka walikuwa na baba huyo huyo mmoja, yaani, baba yetu Isaki.
Również Rebeka, żona naszego przodka Izaaka, urodziła chłopców—bliźniaków.
11 Lakini, hata kabla hao mapacha hawajazaliwa au kufanya jambo lolote jema au baya, ili kwamba kusudi la Mungu la kuchagua lipate kusimama,
Ale zanim się jeszcze urodzili i zanim cokolwiek zrobili—dobrego czy złego—Bóg okazał swoją wolę i wybór,
12 si kwa matendo, bali kwa yeye mwenye kuita, Rebeka aliambiwa, “Yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.”
niezależny od ludzkich czynów. Powiedział Rebece: „Starszy brat będzie służył młodszemu”.
13 Kama vile ilivyoandikwa, “Nimempenda Yakobo, lakini nimemchukia Esau.”
Czytamy w Piśmie: „Ukochałem Jakuba, a odrzuciłem Ezawa”.
14 Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha!
Jaki z tego wniosek? Czy Bóg jest niesprawiedliwy? Absolutnie nie!
15 Kwa maana Mungu alimwambia Mose, “Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
Powiedział przecież Mojżeszowi: „Komu chcę, okazuję miłość, a komu chcę, okazuję litość”.
16 Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu.
Wybór zależy więc nie od tego, który go pragnie lub się o niego stara, ale od Boga, który okazuje łaskę.
17 Kwa maana Maandiko yamwambia Farao, “Nilikuinua kwa kusudi hili hasa, ili nipate kuonyesha uweza wangu juu yako, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.”
Czytamy przecież w Piśmie, że Bóg powiedział faraonowi: „Powołałem cię po to, aby pokazać ci moją moc i aby poznał Mnie cały świat”.
18 Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia yeye atakaye kumhurumia na humfanya mgumu yeye atakaye kumfanya mgumu.
Bóg okazuje więc miłość temu, komu chce, a tego, kogo zechce, czyni upartym.
19 Basi mtaniambia, “Kama ni hivyo, kwa nini basi bado Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kupinga mapenzi yake?”
Wiem, że zaraz powiesz: „Dlaczego więc Bóg ma do ludzi pretensje o to, że zachowują się tak, a nie inaczej? Czy ludzie mogą sprzeciwiać się Jego decyzjom?”.
20 Lakini, ewe mwanadamu, u nani wewe ushindane na Mungu? “Je, kilichoumbwa chaweza kumwambia yeye aliyekiumba, ‘Kwa nini umeniumba hivi?’”
Człowieku! Nawet nie pytaj w ten sposób! Kim jesteś, żeby krytykować Boga? Czy gliniany garnek może powiedzieć garncarzowi: „Dlaczego mnie takim ulepiłeś?”.
21 Je, mfinyanzi hana haki ya kufinyanga kutoka bonge moja vyombo vya udongo, vingine kwa matumizi ya heshima na vingine kwa matumizi ya kawaida?
Czy garncarz nie ma prawa z tej samej gliny ulepić naczynia na specjalne okazje i naczynia do użytku codziennego?
22 Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu?
Bóg, chcąc okazać swój gniew i ogromną moc, cierpliwie znosił ludzi przeznaczonych na gniew i zmierzających do zagłady.
23 Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vile vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake,
Ma też prawo wyrazić swoją dobroć tym, z których uczynił naczynia do przechowywania bogactw swojej chwały.
24 yaani pamoja na sisi, ambao pia alituita, si kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa?
Powołał nas nie tylko spośród Żydów, ale i spośród pogan.
25 Kama vile Mungu asemavyo katika Hosea: “Nitawaita ‘watu wangu’ wale ambao si watu wangu; nami nitamwita ‘mpenzi wangu’ yeye ambaye si mpenzi wangu,”
Dawno temu, zapowiedział bowiem przez proroka Ozeasza: „Nazwę swoim ludem tych, którzy nie należeli do Mnie, i pokocham tych, którzy nie byli kochani”.
26 tena, “Itakuwa hasa mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’”
Pismo mówi także: „Kiedyś mówiono wam, że nie jesteście moim ludem. Teraz zaś zostaniecie nazwani, dziećmi żywego Boga”.
27 Isaya anapiga kelele kuhusu Israeli: “Ingawa idadi ya wana wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaookolewa.
Również prorok Izajasz zapowiedział: „Choćby liczba potomków Izraela była tak wielka, jak ilość ziaren piasku nad morzem, to tylko garstka zostanie ocalona.
28 Kwa kuwa Bwana ataitekeleza hukumu yake duniani kwa haraka na kwa ukamilifu.”
Pan szybko wykona na ziemi swój wyrok i sprawiedliwie zakończy swoje dzieło”.
29 Ni kama vile alivyotabiri Isaya akisema: “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote asingelituachia uzao, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.”
W innym miejscu Izajasz powiedział: „Gdyby Pan nieba nie pozostawił z nas garstki, zostalibyśmy wytraceni jak mieszkańcy Sodomy, i spotkałaby nas ta sama kara, co mieszkańców Gomory”.
30 Kwa hiyo tuseme nini basi? Kwamba watu wa Mataifa ambao hawakutafuta haki, wamepata haki ile iliyo kwa njia ya imani.
Jaki więc płynie z tego wniosek? Taki, że chociaż poganie nie zabiegali o uniewinnienie przez Boga, otrzymali je—przez wiarę.
31 Lakini Israeli, ambao walijitahidi kupata haki kwa njia ya sheria, hawakuipata.
Izrael zaś, pragnąc uzyskać uniewinnienie dzięki Prawu Mojżesza, nie osiągnął go.
32 Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa njia ya imani bali kwa njia ya matendo. Wakajikwaa kwenye lile “jiwe la kukwaza.”
Dlaczego? Bo czynił to nie przez wiarę, ale przez uczynki. Potknęli się o „kamień obrazy”,
33 Kama ilivyoandikwa: “Tazama naweka katika Sayuni jiwe la kukwaza watu na mwamba wa kuwaangusha. Yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”
o którym Pismo mówi: „Kładę na górze Syjon kamień obrazy i skałę, o którą wielu się potknie. Ten jednak, kto mu uwierzy, nie zawiedzie się”.

< Warumi 9 >