< Warumi 8 >
1 Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
Acunakyase, tuhkbäih Khritaw Jesuh üng vekiea phäha mkatnak am ve ti.
2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.
Ngmüimkhya thum naw Jesuh khritaw üngkhyüh lawki xünnak ning jah pe khai. Acuna xünnak naw mkhyekatnak ja thihnak üngkhyüh ning jah mhlät pängki.
3 Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, yeye aliihukumu dhambi katika mwili,
Ktha ngcekia nghngicim kyase Thum naw am a pawh khawh cun Pamhnam naw a pawh ni. Pamhnam naw nghngicima mäiha amäta Cakpa Jesuh Khritaw tüih law lü ani cun mkhyemsawhki nghngicima mäia law lü mkhyekatnak cun nängeiki.
4 ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
Pamhnam naw a pawh hin ngsungpyunki ngjak'hlü Thum cun mimi üng kümkawi lü mimi Ngmüimkhya üng xüng. Acun hin nghngicima mtisa lama am kya.
5 Kwa maana wale wanaoishi kwa kuufuata mwili huziweka nia zao katika vitu vya mwili, lakini wale wanaoishi kwa kufuata Roho, huziweka nia zao katika mambo ya Roho.
Pumsa thuma vekie naw mtisa lama ami mlung takie; Ngmüimkhya thuma vekie naw Ngmüimkhya lama ami mlung takie.
6 Kwa maana kuwa na nia ya mwili ni mauti, bali kuwa na nia inayoongozwa na Roho ni uzima na amani.
Pumsa lama mlung tak cun thihnaka kyaki, Ngmüimkhya lama mlung tak cun xünnak ja dim’yenaka kyaki.
7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Acunakyase, mtisa thum üng xün law üng Pamhnama yea kya lawki he. Pamhnam thum am läk u lü a läka pi am läk khawh u.
8 Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu.
Acunakyase, mtisa thuma vekie naw, Pamhnam am jesak thei u.
9 Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu yeyote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo.
Cunsepi, Pamhnama Ngmüimkhya nangmi üng ve kcangkia akya üng mtisa üng am ve u lü, Ngmüimkhya üng nami veki ni. Cunsepi, u pi Khritawa Ngmüimkhya am taki cun ania khyanga am kya.
10 Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki.
Cunsepi, Khritaw nangmi üng a ve üng, mkhyekatnaka phäha thi khai mtisa pi Pamhnam am nami ngsungpyunkia kyase Ngmüimkhya cun nami xüngnaka kyaki.
11 Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
Jesuh thihnak üngkhyüh mtho bekia Pamhnama Ngmüimkhya nangmi üng a ve ta, Khritaw thihnak üngkhyüh mtho beki nami k'uma veki ania Ngmüimkhya naw thi theikia nami mtisa üngpi xünnak ning jah pe khai.
12 Kwa hiyo ndugu zangu, sisi tu wadeni, si wa mwili, ili tuishi kwa kuufuata mwili,
Acunakyase, ka püie aw, mi mta veki, lüpi mtisa thuma a hlüeia mi xün khaia am kya.
13 kwa maana mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini kama mkiyaua matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.
Mtisa thuma nami ve üng nami thi khai; cunsepi, mtisa bilawhe cun Ngmüimkya am nami ja thihsak üng nami xüng khai.
14 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.
Pamhnama Ngmüimkya naw a jah khyüisawe cun Pamhnama caa kyakie.
15 Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa iwaleteayo tena hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambaye kwa yeye twalia, “Abba, yaani, Baba,”
Pamhnam naw a ning jah peta Ngmüimkhya naw kyühnak ja mpya kyanak be am ning jah pe. Lüpi Ngmüimkhya naw Pamhnama ca thawnnak ja “ka Pa, ka Pa” ti lü ngkhünak vaia ngmüimkhyaa johit ning jah petki.
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu.
Acuna Ngmüimkya Ngcim kung naw mi ngmüimkya üng Pamhnama caea mi kyaki ti cun jah ksingsaki;
17 Hivyo, ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja naye tupate pia kutukuzwa pamoja naye.
A caea mi kyak üng a khyangea phäh a tak khawhthem mi yah khai. Pamhnam naw Khritaw üng a tak pet khawhthem pi mi yah khai isetiakyaküng Khritawa khuikhanak pi mi khameipüi lü a hlüngtainak pi mi yümeipüi khai.
18 Nayahesabu mateso yetu ya wakati huu kuwa si kitu kulinganisha na utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
Tuhkbäih khuikhanake hin, malama hlüngtainak ngdang law khai üng am jah mtäng phyaki ni.
19 Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu.
A mhnünmcenge naküt naw äpeinak am, Pamhnama caea ngdang lawnak vai k'äihkie.
20 Kwa kuwa viumbe vyote viliwekwa chini ya ubatili, si kwa chaguo lao, bali kwa mapenzi yake yeye aliyevitiisha katika tumaini,
A mhnünmcenge naw ami vecawh ning ami mkhyüh hin ami hlüeia am kya lüpi Pamhnam naw acukba a hlüeia kyaki. Lüpi äpeinak veki,
21 ili kwamba viumbe vyote vipate kuwekwa huru kutoka kwa utumwa wa kuharibika na kupewa uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
A mhnünmcenge kung pi pyüpyenaka mpya üngka naw jah mhläta kya khai, Pamhnama caea hlüngtaikia lätnak yah hnga khaiea kyaki.
22 Kwa maana twajua ya kuwa hata sasa viumbe vyote vimekuwa vikilia kwa maumivu kama utungu wa mwanamke wakati wa kuzaa.
A mhnünmcenge naküt tuhvei cäpa ngko u lü na hmi law khaia nghnumia mäiha jah msomhlei u lü vekie tia mi ksingki.
23 Wala si hivyo viumbe peke yao, bali hata sisi ambao ndio matunda ya kwanza ya Roho, kwa ndani tunalia kwa uchungu tukisubiri kwa shauku kufanywa wana wa Mungu, yaani, ukombozi wa miili yetu.
Mhnünmceng däka am kyase, Pamhnam naw amdanga a jah yeta Ngmüimkhya mi taki pi mi mlung k'uma mi ngkoki. Pamhnama caa mi kyaknak vai ja a mhnünmcenge a jah mhlät vai pi mi k'äihei sihki.
24 Kwa kuwa tuliokolewa kwa tumaini hili. Lakini kama kinachotumainiwa kikionekana hakiwi tumaini tena. Je, kuna mtu anayetumaini kupata kitu alicho nacho tayari?
Äpeinak am küikyannak mi yah ve; cunsepi, hmu u lü äpei cun äpeinaka am kya. Khyang naw a hmuh thei cun ihawkba mi äpei khai ni?
25 Lakini tunapotumaini kupata kitu ambacho hatuna, basi twakingojea kwa saburi.
Am mi hmuh thei mi äpei üng, mlung msaünak am mi k'äih khai.
26 Vivyo hivyo, Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo. Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioweza kutamkwa.
Acun käna, Ngmüimkhya naw am mi kyannake üng ja kpüiki. Mi ktaiyü üng ihawkba ktaiyü vai tia am mi ksing. Cunsepi, mi ktaiyü üng ngthu üng am pyen theia ngkonak am Ngmüimkhya naw ngko lü jah ktaiyü peki.
27 Naye Mungu aichunguzaye mioyo, anaijua nia ya Roho, kwa sababu Roho huwaombea watakatifu sawasawa na mapenzi ya Mungu.
Acunüng, Mi mlung jah teng lü Ngmüimkhya naw i cungaiki ti cun ksingki, isetiakyaküng khyangea kcaha Pamhnama veia a ktaiyü hin Pamhnama ngjak'hlüa kyaki.
28 Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
Avan üng atänga Pamhnam mhläkphyanakie, a titänga a jah khüea phäha akdaw vaia biloki tia mi ksingki.
29 Maana wale Mungu aliowajua tangu mwanzo, pia aliwachagua tangu mwanzo, wapate kufanana na mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
A jah ksing pänge cun amäta a ca mäiha ve khaiea a jah na mhnün päng, a Cakpa cun bena khawhahea ksunga ca kcüka a kya lawnak thei vaia kyaki.
30 Nao wale Mungu aliotangulia kuwachagua, akawaita, wale aliowaita pia akawahesabia haki, nao wale aliowahesabia haki, pia akawatukuza.
Acunakyase a jah na phyäi pänge ni a jah khü; a jah khüe ni amät am a jah ngsungpyunsak; a jah ngsungpyunsak pänge ni a jah mhlünmtai.
31 Tuseme nini basi kuhusu haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani awezaye kuwa kinyume chetu?
Acunüng a hina ngthue üng i mi pyen thei khai? Pamhnam mimi phäha a ve üng u naw jah tu thei khai ni?
32 Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja naye?
Amäta Cakpa pi am kpamei lü mi vana phäha jah peki naw, avan naküt amdanga am jah pet sih khai aw?
33 Ni nani atakayewashtaki wale ambao Mungu amewateua? Ni Mungu mwenyewe ndiye mwenye kuwahesabia haki.
Pamhnama xüa khyange cun u naw jah ksekha na thei khai ni? Pamhnam amät kung naw am mkhyekat u a ti.
34 Ni nani basi atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu aliyekufa, naam, zaidi ya hayo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yuko mkono wa kuume wa Mungu, naye pia anatuombea.
U naw jah mkatei thei khai ni? Khritaw Jesuh naw am jah mkatei. Thi lü, thi däkia am kya lü, thihnak üngka naw tho law be lü Pamhnama khet lama ve lü jah ktaiyü peki cun Khritawa kyaki ni.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?
Khritawa mhläkphyanak üngka naw u naw ja mtai thei khai aw? Khuikhatnak naw pi kyase, khaknak naw pi kyase, mkhuimkhanak naw pi kyase, cawixainak naw pi kyase, akpuma venak naw pi kyase, kyühkyawknak naw pi kyase, thihnak naw pi kyase, jah mtai thei khai aw?
36 Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
“Nanga phäha anglät se thihnak vai üng kami veki; hnim vaia toca mäia ami jah pawh” tia Cangcim naw pyenki.
37 Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
Am jah mtai, jah jawngnakia a bäkhäknaka phäha acune naküt kami jah näng päng ni.
38 Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa sio mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo,
Isetiakyaküng, thihnaka pi kyase, xünaka pi kyase, khankhaw ngsäa pi kyase, khawyai ksea pi kyase, khankhaw anaa pi kyase, tuhkbäih üngkaea pi kyase, tuha ve law khaiea pi kyase,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote zitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu, Bwana wetu.
ak’hlünga pi kyase, aknema pi kyase, mhnünmceng naküt üngka i naw pi, mi Bawipa Jesuh Khritaw vei mi yaha Pamhnama mhläkphyanak üngka naw am jah mtai thei khai tia akcanga ka ksingki.