< Warumi 7 >
1 Ndugu zangu (sasa ninasema na wale wanaoijua sheria), je, hamjui ya kwamba sheria ina mamlaka tu juu ya mtu wakati akiwa hai?
Do you not know, brethren, (for I speak to them who know law, ) that the law has dominion over a man as long as he lives?
2 Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mumewe wakati akiwa hai, lakini yule mume akifa, yule mwanamke amefunguliwa kutoka sheria ya ndoa.
For the married woman is bound, by law, to her husband as long as he lives; but if the husband be dead, she is released from the law of her husband.
3 Hivyo basi, kama huyo mwanamke ataolewa na mwanaume mwingine wakati mumewe akiwa bado yuko hai, ataitwa mzinzi. Lakini kama mumewe akifa, mwanamke huyo hafungwi tena na sheria ya ndoa, naye akiolewa na mtu mwingine haitwi mzinzi.
If, then, indeed, while her husband lives, she be married to another, she shall be called an adulteress: but if her husband be dead, she is free from the law; so that she is not an adulteress, though married to another husband.
4 Vivyo hivyo, ndugu zangu, ninyi mmeifia sheria kwa njia ya mwili wa Kristo, ili mweze kuwa mali ya mwingine, yeye ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu, ili tupate kuzaa matunda kwa Mungu.
Thus, my brethren, you also have become dead to the law, by the body of Christ, that you may be married to another, who rose from the dead, that we may bring forth fruit to God.
5 Kwa maana tulipokuwa tunatawaliwa na asili ya dhambi, tamaa za dhambi zilizochochewa na sheria zilikuwa zikitenda kazi katika miili yetu, hivyo tulizaa matunda ya mauti.
For when we were in the flesh, our sinful passions which were through the law, wrought effectually in our members, to bring forth fruit to death.
6 Lakini sasa, kwa kufia kile kilichokuwa kimetufunga kwanza, tumewekwa huru kutokana na sheria ili tutumike katika njia mpya ya Roho, wala si katika njia ya zamani ya sheria iliyoandikwa.
But now, having died with Christ, we are released from the law, by which we were held in bondage; so that we may serve God in newness of spirit, and not in oldness of the letter.
7 Tuseme nini basi? Kwamba sheria ni dhambi? La, hasha! Lakini, isingekuwa kwa sababu ya sheria, nisingalijua dhambi. Nisingalijua kutamani ni nini kama sheria haikusema, “Usitamani.”
What shall we say, then? Is the law sin? By no means. Indeed, I had not known sin, except by the law. For I had not known even inordinate desire, unless the law had said, "You shall not lust."
8 Lakini dhambi kwa kupata nafasi katika amri, hii ikazaa ndani yangu kila aina ya tamaa. Kwa maana pasipo sheria, dhambi imekufa.
But sin, taking occasion by the commandment, wrought in me all manner of inordinate desire: for without the law sin is dead.
9 Wakati fulani nilikuwa hai pasipo sheria, lakini amri ilipokuja, dhambi ikawa hai, nami nikafa.
For I was alive, once, without the law: but when the commandment came, sin revived, but I died.
10 Nikaona kwamba ile amri iliyokusudiwa kuleta uzima, ilileta mauti.
Yes, the commandment which was for live, the very same was found to be death to me.
11 Kwa maana dhambi kwa kupata nafasi katika amri, ilinidanganya, na kupitia katika hiyo amri, ikaniua.
For sin, taking occasion by the commandment, deceived me, and by it slew me.
12 Hivyo basi, sheria yenyewe ni takatifu, na amri ni takatifu na ya haki, tena ni njema.
Wherefore, the law is holy, and the commandment holy, just, and good.
13 Je, kile kilicho chema basi kilikuwa mauti kwangu? La, hasha! Lakini ili dhambi itambuliwe kuwa ni dhambi, ilileta mauti ndani yangu kupitia kile kilichokuwa chema, ili kwa njia ya amri dhambi izidi kuwa mbaya kupita kiasi.
Has, then, that which is good become death to me? By no means. But sin becomes death, in order that it might manifest itself, causing death to me by that which is good: so that sin, (through the commandment, ) might be an exceedingly great sinner.
14 Kwa maana tunajua kwamba sheria ni ya kiroho, lakini mimi ni wa kimwili nikiwa nimeuzwa kwenye utumwa wa dhambi.
Besides, we know that the law is spiritual: but I am carnal, sold under sin.
15 Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia.
For that which I do, I do not approve; since it is not what I desire that I do: but I do that which I hate.
16 Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, ni kwamba ninakubali kuwa sheria ni njema.
If, now, I do that which I do not desire, I consent to the law that it is good.
17 Lakini, kwa kweli si mimi tena nitendaye lile nisilotaka bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
But now it is no longer I myself who do this; but sin which dwells in me.
18 Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna jema lolote likaalo ndani yangu, yaani, katika asili yangu ya dhambi. Kwa kuwa nina shauku ya kutenda lililo jema, lakini siwezi kulitenda.
For I know that in me, that is, in my flesh, there dwells no good thing: for to desire what is good, is easy for me; but to do it, I find difficult.
19 Sitendi lile jema nitakalo kutenda, bali lile baya nisilolitaka, ndilo nitendalo.
For the good which I desire, that I do not: but the evil which I desire not, that I do.
20 Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
Now, if I do that which I do not desire, it is no longer I who do it; but sin, which dwells in me.
21 Hivyo naiona sheria ikitenda kazi. Ninapotaka kutenda jema, jambo baya liko papo hapo.
I find, then, that it is a law to me, when desirous to do good, that evil is near me.
22 Kwa maana katika utu wangu wa ndani naifurahia sheria ya Mungu.
For I take pleasure in the law of God, as to the inner man:
23 Lakini ninaona kuna sheria nyingine inayotenda kazi katika viungo vya mwili wangu inayopigana vita dhidi ya ile sheria ya akili yangu. Sheria hii inanifanya mateka wa ile sheria ya dhambi inayofanya kazi katika viungo vya mwili wangu.
but I perceive another law, in my members, warring against the law of my mind, and making me a captive to the law of sin, which is in my members.
24 Ole wangu mimi maskini! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
Wretched man that I am! who shall deliver me from this body of death?
25 Ashukuriwe Mungu kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu! Hivyo basi, mimi mwenyewe kwa akili zangu ni mtumwa wa sheria ya Mungu, lakini katika asili ya dhambi ni mtumwa wa sheria ya dhambi.
I thank God, through Jesus Christ our Lord! Wherefore, then, indeed, I myself serve, with my mind, the law of God; but with the flesh, the law of sin.