< Warumi 6 >

1 Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka?
What then shall we say? Shall we continue to abound in sin, in order that grace may come to abound?
2 La hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutawezaje kuendelea kuishi tena katika dhambi?
No indeed; how shall we who have died to sin still go on living in it any longer?
3 Au hamjui ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
For do you not know that all of us who have been baptized into Jesus Christ, have been baptized into his death?
4 Kwa hiyo tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa utukufu wa Baba, vivyo hivyo sisi nasi pia tupate kuenenda katika upya wa uzima.
We have been buried together with him, then, through baptism into his death, in order that just as Christ was raised from the dead through the glory of the Father, so also we should live in a newness of life.
5 Kwa maana ikiwa tumeungana naye katika mauti yake, bila shaka tutaungana naye katika ufufuo wake.
For if we have become united with him in the likeness of his death, so we shall also be united with him in the likeness of his resurrection.
6 Kwa maana twajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja naye ili ule mwili wa dhambi upate kuangamizwa, nasi tusiendelee kuwa tena watumwa wa dhambi.
For this we know, that our old self was crucified with Christ, in order that the slave of sin might be destroyed; so that we should no longer be in slavery to sin -
7 Kwa maana mtu yeyote aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
for he who is dead is set free from sin.
8 Basi ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye.
Now if we have died with Christ, we believe that we shall also live with him;
9 Kwa maana tunajua kwamba Kristo, kwa sababu alifufuliwa kutoka kwa wafu, hawezi kufa tena; mauti haina tena mamlaka juu yake.
knowing that Christ, being raised from the dead, dies no more; death has no more dominion over him.
10 Kifo alichokufa, aliifia dhambi mara moja tu, lakini uzima alio nao anamwishia Mungu.
For the death that he died, he died unto sin once for all; but the life that he lives he is living unto God.
11 Vivyo hivyo, jihesabuni wafu katika dhambi lakini mlio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Even so count yourselves also to be dead unto sin, but alive unto God in Christ Jesus.
12 Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya.
Therefore let not sin rule as king in your mortal body, compelling you to obey its lusts.
13 Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu kwake kama vyombo vya haki.
Do not continue to present any part of your body to sin to be used as a weapon of unrighteousness. On the contrary, be presenting yourselves to God, as alive from the dead, and the various parts of your bodies to be used as weapons of righteousness.
14 Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.
For sin shall not lord it over you; for you are not under the rule of law, but under the rule of grace.
15 Ni nini basi? Je, tutende dhambi kwa kuwa hatuko chini ya sheria bali chini ya neema? La, hasha!
What then? Shall we commit an act of sin because we are not under law, but under grace? Certainly not.
16 Je, hamjui kwamba mnapojitoa kwa mtu yeyote kama watumwa watiifu, ninyi ni watumwa wa yule mnayemtii, aidha watumwa wa dhambi, ambayo matokeo yake ni mauti, au watumwa wa utii ambao matokeo yake ni haki?
Do you not know that when you surrender yourselves as slaves to any one to obey him, you are his slaves whom you obey; whether it be sin, whose end is death, or obedience, whose end is righteousness?
17 Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao kwanza mlikuwa watumwa wa dhambi, mmekuwa watii kutoka moyoni kwa mafundisho mliyopewa.
But God be thanked that you who were once the slaves of sin have obeyed from your hearts that type of teaching to which you were appointed;
18 Nanyi, mkiisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mmekuwa watumwa wa haki.
and being set free from sin, you became the slaves of righteousness -
19 Ninasema kwa namna ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wenu wa hali ya asili. Kama vile mlivyokuwa mkivitoa viungo vya miili yenu kama watumwa wa mambo machafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi, hivyo sasa vitoeni viungo vyenu kama watumwa wa haki inayowaelekeza mpate kutakaswa.
I speak in these homely figures because of the weakness of your fleshly nature - just as you once surrendered your faculties into slavery to impurity and to all lawlessness, so now you must surrender your faculties into slavery to righteousness, unto deeds of holiness.
20 Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki.
For when you were the slaves of sin, you were under no subjection to righteousness.
21 Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni mauti.
What harvest-fruit then had you at that time in the things of which you are now ashamed? For the end of those things is death.
22 Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
But now that you have been set free from sin and become slaves of God, the harvest-fruit which you are reaping tends to produce holiness, and it ends is life eternal. (aiōnios g166)
23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)
FOR THE POOR WAGES OF SIN IS DEATH, BUT THE FREE GIFT OF GOD IS ETERNAL LIFE IN CHRIST JESUS, OUR MASTER. (aiōnios g166)

< Warumi 6 >