< Warumi 6 >

1 Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka?
So what shall we say? Shall we continue in the sin so that the grace may abound?
2 La hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutawezaje kuendelea kuishi tena katika dhambi?
Of course not! How can we who died to sin keep on living in it?
3 Au hamjui ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
Or are you unaware that as many of us as were baptized into Christ Jesus were baptized into His death?
4 Kwa hiyo tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa utukufu wa Baba, vivyo hivyo sisi nasi pia tupate kuenenda katika upya wa uzima.
Therefore, we were buried with Him by means of that baptism into that death, so that just as Christ was raised from the dead by means of the Father's glory, we also should walk in newness of life.
5 Kwa maana ikiwa tumeungana naye katika mauti yake, bila shaka tutaungana naye katika ufufuo wake.
Now if we have become united with Him in His death, we will certainly be in His resurrection as well;
6 Kwa maana twajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja naye ili ule mwili wa dhambi upate kuangamizwa, nasi tusiendelee kuwa tena watumwa wa dhambi.
knowing this, that our old self was crucified with Him in order that the body of the sin might be set aside, so that we no longer be enslaved to that sin—
7 Kwa maana mtu yeyote aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
because he who has died has been released from that sin.
8 Basi ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye.
Now since we died with Christ, we believe that we will also live with Him,
9 Kwa maana tunajua kwamba Kristo, kwa sababu alifufuliwa kutoka kwa wafu, hawezi kufa tena; mauti haina tena mamlaka juu yake.
knowing that Christ, having been raised from the dead, cannot die again; death can no longer master Him
10 Kifo alichokufa, aliifia dhambi mara moja tu, lakini uzima alio nao anamwishia Mungu.
—the death He died He died to sin once for all, while the life He lives He lives to God.
11 Vivyo hivyo, jihesabuni wafu katika dhambi lakini mlio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Thus you also, consider yourselves to be dead indeed to the sin, but alive to God in Christ Jesus our Lord.
12 Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya.
Therefore do not let the sin reign in your mortal body, so that you obey it with the body's evil desires
13 Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu kwake kama vyombo vya haki.
—do not present any part of your body to sin as an implement for unrighteousness, but present yourselves to God as those who are alive from the dead, and your body parts to God as implements for righteousness.
14 Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.
Really, sin must not rule over you, because you are not under law but under grace.
15 Ni nini basi? Je, tutende dhambi kwa kuwa hatuko chini ya sheria bali chini ya neema? La, hasha!
What then? Shall we sin because we are not under law but under grace? Of course not!
16 Je, hamjui kwamba mnapojitoa kwa mtu yeyote kama watumwa watiifu, ninyi ni watumwa wa yule mnayemtii, aidha watumwa wa dhambi, ambayo matokeo yake ni mauti, au watumwa wa utii ambao matokeo yake ni haki?
Do you not know that when you offer yourselves to someone to obey them as slaves, you are slaves to the one whom you obey—whether of sin into death, or of obedience into righteousness?
17 Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao kwanza mlikuwa watumwa wa dhambi, mmekuwa watii kutoka moyoni kwa mafundisho mliyopewa.
But thanks be to God that although you used to be the slaves of the sin you wholeheartedly obeyed that pattern of doctrine into which you were delivered.
18 Nanyi, mkiisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mmekuwa watumwa wa haki.
So having been emancipated from the sin, you became enslaved to the righteousness.
19 Ninasema kwa namna ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wenu wa hali ya asili. Kama vile mlivyokuwa mkivitoa viungo vya miili yenu kama watumwa wa mambo machafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi, hivyo sasa vitoeni viungo vyenu kama watumwa wa haki inayowaelekeza mpate kutakaswa.
I continue to speak on a human level because of the weakness of your flesh. Now just as you used to present your body parts as slaves to uncleanness, and to ever increasing lawlessness, so now present your body parts as slaves to righteousness with a view to sanctification.
20 Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki.
For when you were slaves to the sin, you were ‘free’ from the righteousness.
21 Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni mauti.
So what ‘fruit’ did you have at that time from the things you are now ashamed of? The end of those things is death!
22 Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
But now, having been emancipated from the sin, and having become enslaved to God, you have your ‘fruit’ into sanctification—and the end is eternal life! (aiōnios g166)
23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)
Because the wages of sin is death, but the gracious gift of God is eternal life in Christ Jesus our Lord. (aiōnios g166)

< Warumi 6 >