< Warumi 5 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Będąc tedy usprawiedliwieni z wiary, pokój mamy z Bogiem przez Pana naszego Jezusa Chrystusa;
2 ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
Przez któregośmy też przystęp otrzymali wiarą ku łasce, w której stoimy i chlubimy się nadzieją chwały Bożej.
3 Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
A nie tylko to, ale się też chlubimy z ucisków, wiedząc, iż ucisk cierpliwość sprawuje,
4 nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
A cierpliwość doświadczenie, a doświadczenie nadzieję,
5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
A nadzieja nie pohańbia, przeto iż miłość Boża rozlana jest w sercach naszych przez Ducha Świętego, który nam jest dany.
6 Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
Albowiem Chrystus, gdy jeszcze byliśmy mdłymi, według czasu umarł za niepobożne.
7 Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
Choć ledwie by kto umarł za sprawiedliwego; wszakże za dobrego snaćby się kto umrzeć ważył.
8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
Lecz zaleca Bóg miłość swoję ku nam, że gdy jeszcze byliśmy grzesznymi, Chrystus za nas umarł.
9 Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
Daleko tedy więcej teraz usprawiedliwieni będąc krwią jego, zachowani będziemy przez niego od gniewu.
10 Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
Bo jeźliże będąc nieprzyjaciołmi, pojednaniśmy z Bogiem przez śmierć Syna jego; daleko więcej będąc pojednani, zachowani będziemy przez żywot jego.
11 Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
A nie tylko to, ale się też chlubimy Bogiem przez Pana naszego Jezusa Chrystusa, przez któregośmy teraz pojednanie otrzymali.
12 Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
Przetoż jako przez jednego człowieka grzech wszedł na świat, a przez grzech śmierć; tak też na wszystkich ludzi śmierć przyszła, ponieważ wszyscy zgrzeszyli.
13 kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
Albowiem aż do zakonu grzech był na świecie; ale grzech nie bywa przyczytany, gdy zakonu nie masz.
14 Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
Lecz śmierć królowała od Adama aż do Mojżesza i nad tymi, którzy nie zgrzeszyli, na podobieństwo przestępstwa Adamowego, który jest wzorem onego, który miał przyjść.
15 Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
Ale nie jako upadek, tak i dar z łaski; albowiem jeźli przez upadek jednego wiele ich pomarło, daleko więcej łaska Boża i dar z łaski onego jednego człowieka Jezusa Chrystusa na wiele ich opływała.
16 Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
A dar nie jest taki, jako to, co przyszło przez jednego, który zgrzeszył. Albowiem wina jest z jednego upadku ku potępieniu, ale dar z łaski z wielu upadków ku usprawiedliwieniu.
17 Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
Albowiem jeźli dla jednego upadku śmierć królowała przez jednego, daleko więcej, którzy obfitość onej łaski i dar sprawiedliwości przyjmują, w żywocie królować będą przez tegoż jednego Jezusa Chrystusa.
18 Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
Przetoż tedy jako przez jednego upadek na wszystkich ludzi przyszła wina ku potępieniu; tak też przez jednego usprawiedliwienie na wszystkich ludzi przyszedł dar ku usprawiedliwieniu żywota.
19 Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
Bo jako przez nieposłuszeństwo jednego człowieka wiele się ich stało grzesznymi; tak przez posłuszeństwo jednego człowieka wiele się ich stało sprawiedliwymi.
20 Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
A zakon przytem nastąpił, aby obfitował grzech; lecz gdzie się grzech rozmnożył, tam łaska tem więcej obfitowała.
21 ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)
Aby jako grzech królował ku śmierci, tak też aby łaska królowała przez sprawiedliwość ku żywotowi wiecznemu przez Jezusa Chrystusa, Pana naszego. (aiōnios g166)

< Warumi 5 >