< Warumi 5 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
BECAUSE, then, we are justified by faith, we have peace with Aloha through our Lord Jeshu Meshiha.
2 ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
And by him we have been admitted through faith into this grace in which we stand, and exult in hope of the glory of Aloha.
3 Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
And not thus only, but also in afflictions we exult; for we know that affliction perfecteth patience in us,
4 nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
and patience experience, and experience hope:
5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
but hope maketh us not ashamed, because the love of Aloha is shed forth upon our hearts by the Spirit of Holiness who is given to us.
6 Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
But if the Meshiha on account of our infirmity in this time for the wicked hath died:
7 Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
for hardly for the wicked one dieth; for on account of the good one may perhaps dare to die.
8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
Nevertheless Aloha hath manifested his love for us, in that, when we were sinners, the Meshiha for us died:
9 Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
how much more, then, shall we be now justified through his blood, and by him be delivered from wrath?
10 Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
For if, while we were adversaries, Aloha was reconciled with us through the death of his Son, how much more, then, in reconciliation with him, shall we be saved by his life?
11 Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
And not thus only, but we also exult in Aloha through our Lord Jeshu Meshiha, by whom we have now received the reconciliation.
12 Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
As by one man sin entered into the world, and by sin death, so death hath passed upon all men through this, that all have sinned.
13 kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
For until the law, sin, while it was in the world, was not reckoned sin, because the law was not;
14 Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
yet death reigned from Adam until Musha on them also who had not sinned after the manner of the transgression of the law of Adam, who was the type of him who was to be.
15 Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
But not as was the fall, so is the gift; for if, on account of the fall of one, many died, how much more the grace of Aloha, and his gift, for the sake of one man, Jeshu Meshiha, in many will abound?
16 Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
And not as the transgression of one, so is the gift; for the judgment that was by one was unto condemnation, but the gift (which saves) from many sins was unto righteousness.
17 Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
For if because of the transgression of one death was made to reign, much more (shall) they who receive the abundance of the grace and of the gift and of righteousness, reign in life by one, Jeshu Meshiha.
18 Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
As then on account of the transgression of one was the condemnation of all men, so, on account of the righteousness of one shall there be acquittal unto the life of all men.
19 Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
For as on account of the disobedience of one man many became sinners, so also on account of the obedience of one many became righteous.
20 Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
But the entrance which was of the law, (made) sin to increase; and where sin increased, there grace hath abounded:
21 ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)
that as sin hath reigned in death, so grace might reign in righteousness unto the life which is eternal, by the hand of our Lord Jeshu Meshiha. (aiōnios g166)

< Warumi 5 >