< Warumi 5 >
1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Therefore, having been justified by faith, let us be at peace with God, through our Lord Jesus Christ.
2 ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
For through him we also have access by faith to this grace, in which we stand firm, and to glory, in the hope of the glory of the sons of God.
3 Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
And not only that, but we also find glory in tribulation, knowing that tribulation exercises patience,
4 nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
and patience leads to proving, yet truly proving leads to hope,
5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
but hope is not unfounded, because the love of God is poured forth in our hearts through the Holy Spirit, who has been given to us.
6 Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
Yet why did Christ, while we were still infirm, at the proper time, suffer death for the impious?
7 Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
Now someone might barely be willing to die for the sake of justice, for example, perhaps someone might dare to die for the sake of a good man.
8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
But God demonstrates his love for us in that, while we were yet sinners, at the proper time,
9 Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
Christ died for us. Therefore, having been justified now by his blood, all the more so shall we be saved from wrath through him.
10 Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
For if we were reconciled to God through the death of his Son, while we were still enemies, all the more so, having been reconciled, shall we be saved by his life.
11 Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
And not only that, but we also glory in God through our Lord Jesus Christ, through whom we have now received reconciliation.
12 Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
Therefore, just as through one man sin entered into this world, and through sin, death; so also death was transferred to all men, to all who have sinned.
13 kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
For even before the law, sin was in the world, but sin was not imputed while the law did not exist.
14 Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
Yet death reigned from Adam until Moses, even in those who have not sinned, in the likeness of the transgression of Adam, who is a figure of him who was to come.
15 Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
But the gift is not entirely like the offense. For though by the offense of one, many died, yet much more so, by the grace of one man, Jesus Christ, has the grace and gift of God abounded to many.
16 Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
And the sin through one is not entirely like the gift. For certainly, the judgment of one was unto condemnation, but the grace toward many offenses is unto justification.
17 Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
For though, by the one offense, death reigned through one, yet so much more so shall those who receive an abundance of grace, both of the gift and of justice, reign in life through the one Jesus Christ.
18 Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
Therefore, just as through the offense of one, all men fell under condemnation, so also through the justice of one, all men fall under justification unto life.
19 Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
For, just as through the disobedience of one man, many were established as sinners, so also through the obedience of one man, many shall be established as just.
20 Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
Now the law entered in such a way that offenses would abound. But where offenses were abundant, grace was superabundant.
21 ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios )
So then, just as sin has reigned unto death, so also may grace reign through justice unto eternal life, through Jesus Christ our Lord. (aiōnios )