< Warumi 5 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Therefore, being justified by faith, we have peace with God through our Lord Jesus Christ,
2 ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
through whom we have had access, by faith, into this grace in which we stand; and we rejoice in hope of the glory of God.
3 Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
And not only so, but we rejoice in afflictions also; because we know that affliction produces patience,
4 nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
and patience, an approved character, and an approved character, hope;
5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
and this hope disappoints us not; because the love of God is poured abundantly into our hearts through the Holy Spirit that is given to us.
6 Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
For when we were yet without strength, at the appointed time, Christ died for the ungodly.
7 Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
For hardly, indeed, will one die for a just man; yet, perhaps, for the good man some one would even dare to die.
8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
But God makes known his love to us in this, that while we were yet sinners, Christ died for us:
9 Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
much more, then, since we are now justified by his blood, we shall be saved from the wrath through him.
10 Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
For if, while we were enemies, we were reconciled to God by the death of his Son, much more, having been reconciled, shall we be saved by his life.
11 Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
And not only so, but we rejoice in God through our Lord Jesus Christ, by whom we have now received the reconciliation.
12 Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
For this reason, as by one man sin entered into the world, and by his sin, death; and so death passed through to all men, because all have sinned:
13 kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
for till the law, sin was in the world; but sin is not charged where there is no law.
14 Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
Yet death reigned from Adam to Moses, even over them that did not sin in the likeness of Adam’s transgression, who is the type of him that was to come.
15 Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
But the favor bestowed is not, in all respects, like the offense: for if, by the offense of one, the many have died, much more have the grace of God and the gift which is by the grace of the one man Jesus Christ, been made abundant for the many.
16 Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
And the gift is not like the sentence that came through one who sinned: for the sentence to condemnation was because of one offense; but the favor bestowed in order to justification, is because of many offenses.
17 Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
For if, by one man’s offense, death has reigned through that one, much more shall those who receive the abundance of the grace, and of the gift of righteousness, reign in life through the one, who is Jesus Christ.
18 Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
Therefore, as, by one offense, sentence came on all men to condemnation, so, also, by one act of righteousness, the gift has come on all men to justification of life.
19 Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
For as by the disobedience of the one man the many have been made sinners, so, also, by the obedience of the one, the many shall be made righteous.
20 Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
But, besides the first offense, law was introduced, in order that offenses might abound: but where sin abounded, grace did much more abound:
21 ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)
that as sin has reigned, ending in death, so might grace reign by justification, ending in life eternal, through Jesus Christ our Lord. (aiōnios g166)

< Warumi 5 >