< Warumi 4 >

1 Tuseme nini basi, kuhusu Abrahamu baba yetu kwa jinsi ya mwili: yeye alipataje kujua jambo hili?
What shall we saye then that Abraham oure father as pertayninge to ye flesshe dyd finde?
2 Kwa maana ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo, basi, anacho kitu cha kujivunia, lakini si mbele za Mungu.
If Abraham were iustified by dedes the hath he wherin to reioyce: but not with god.
3 Kwa maana Maandiko yasemaje? “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
For what sayth the scripture? Abraham beleved god and it was counted vnto him for rightewesnes.
4 Basi mtu afanyapo kazi, mshahara wake hauhesabiwi kwake kuwa ni zawadi, bali ni haki yake anayostahili.
To him that worketh is the rewarde not reckened of favour: but of duty.
5 Lakini kwa mtu ambaye hafanyi kazi na anamtumaini Mungu, yeye ambaye huwahesabia waovu haki, imani yake inahesabiwa kuwa haki.
To him that worketh not but beleveth on him that iustifieth the vngodly is his fayth counted for rightewesnes.
6 Daudi pia alisema vivyo hivyo aliponena juu ya baraka za mtu ambaye Mungu humhesabia haki pasipo matendo:
Even as David describeth the blessedfulnes of the man vnto whom god ascribeth rihgtewesnes without dedes.
7 “Wamebarikiwa wale ambao wamesamehewa makosa yao, ambao dhambi zao zimefunikwa.
Blessed are they whose vnrightewesnes are forgeven and whose synnes are covered.
8 Heri mtu yule Bwana hamhesabii dhambi zake.”
Blessed is that ma to whom the Lorde imputeth not synne.
9 Je, huku kubarikiwa ni kwa wale waliotahiriwa peke yao, au pia na kwa wale wasiotahiriwa? Tunasema, “Imani ya Abrahamu ilihesabiwa kwake kuwa haki.”
Came this blessednes then vpon the circumcised or vpon the vncircucised? We saye verely how that fayth was rekened to Abraham for rightewesnes.
10 Je, ni lini basi ilipohesabiwa kwake kuwa haki? Je, ilikuwa kabla au baada ya kutahiriwa kwake? Haikuwa baada, ila kabla hajatahiriwa.
How was it rekened? in the tyme of circumcision? or in the tyme before he was circumcised? Not in tyme of circucision: but when he was yet vncircumcised.
11 Alipewa ishara ya tohara kuwa muhuri wa haki aliyokuwa nayo kwa imani hata alipokuwa bado hajatahiriwa. Kusudi lilikuwa kumfanya baba wa wote wale waaminio pasipo kutahiriwa na ambao wamehesabiwa haki.
And he receaved the signe of circumcision as a seale of yt rightewesnes which is by fayth which fayth he had yet beynge vncircucised: that he shuld be the father of all them that beleve though they be not circumcised that rightewesnes myght be imputed to them also:
12 Vivyo hivyo awe baba wa wale waliotahiriwa ambao si kwamba wametahiriwa tu, bali pia wanafuata mfano wa imani ambayo Baba yetu Abrahamu alikuwa nayo kabla ya kutahiriwa.
and that he myght be the father of the circumcised not because they are circumcised only: but because they walke also in the steppes of that fayth yt was in oure father Abraham before the tyme of circumcision.
13 Kwa maana ile ahadi kwamba angeurithi ulimwengu haikuja kwa Abrahamu au kwa wazao wake kwa njia ya sheria bali kwa njia ya haki ipatikanayo kwa imani.
For the promes that he shuld be the heyre of the worlde was not geven to Abraha or to his seed thorow the lawe: but thorow ye rightewesnes which cometh of fayth.
14 Kwa maana ikiwa wale waishio kwa sheria ndio warithi, imani haina thamani na ahadi haifai kitu,
For yf they which are of the lawe be heyres then is fayth but vayne and the promes of none effecte.
15 kwa sababu sheria huleta ghadhabu. Mahali ambapo hakuna sheria hakuna makosa.
Because the lawe causeth wrathe. For where no lawe is there is no trasgression.
16 Kwa hiyo, ahadi huja kwa njia ya imani, ili iwe ni kwa neema, na itolewe kwa wazao wa Abrahamu, si kwa wale walio wa sheria peke yao, bali pia kwa wale walio wa imani ya Abrahamu. Yeye ndiye baba yetu sisi sote.
Therfore by fayth is the inheritauce geven that it myght come of faveour: and the promes myght be sure to all the seed. Not to them only which are of the lawe: but also to them which are of the fayth of Abraham which is the father of vs all.
17 Kama ilivyoandikwa: “Nimekufanya wewe kuwa baba wa mataifa mengi.” Yeye ni baba yetu mbele za Mungu, ambaye yeye alimwamini, yule Mungu anaye fufua waliokufa, na kuvitaja vile vitu ambavyo haviko kana kwamba vimekwisha kuwako.
As it is wrytten: I have made the a father to many nacions even before god whom thou hast beleved which quyckeneth the deed and called those thinges which be not as though they were.
18 Akitarajia yasiyoweza kutarajiwa, Abrahamu akaamini, akawa baba wa mataifa mengi, kama alivyoahidiwa kwamba, “Uzao wako utakuwa mwingi mno.”
Which Abraham contrary to hope beleved in hope that he shuld be the father of many nacions accordynge to that which was spoken:
19 Abrahamu hakuwa dhaifu katika imani hata alipofikiri juu ya mwili wake, ambao ulikuwa kama uliokufa, kwani umri wake ulikuwa unakaribia miaka mia moja, au alipofikiri juu ya ufu wa tumbo la Sara.
So shall thy seed be. And he faynted not in the fayth nor yet consydered hys awne body which was now deed even when he was almost an hondred yeare olde: nether yet that Sara was past chyldeberinge.
20 Lakini Abrahamu hakusitasita kwa kutokuamini ahadi ya Mungu, bali alitiwa nguvu katika imani yake na kumpa Mungu utukufu,
He stackered not at the promes of God thorow vnbelefe: but was made stronge in the fayth and gave honour to God
21 akiwa na hakika kabisa kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kutimiza lile aliloahidi.
full certifyed that what he had promised that he was able to make good.
22 Hii ndio sababu, “ilihesabiwa kwake kuwa haki.”
And therfore was it reckened to him for rightewesnes.
23 Maneno haya “ilihesabiwa kwake kuwa haki,” hayakuandikwa kwa ajili yake peke yake,
It is not written for him only that it was reckened to him for rightewesnes:
24 bali kwa ajili yetu sisi pia ambao Mungu atatupa haki, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu.
but also for vs to whom it shalbe counted for rightewesnes so we beleve on him that raysed vp Iesus oure Lorde from deeth.
25 Alitolewa afe kwa ajili ya dhambi zetu, naye alifufuliwa kutoka mauti ili tuhesabiwe haki.
Which was delivered for oure synnes and rose agayne forto iustifie vs.

< Warumi 4 >