< Warumi 3 >

1 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
Qual é logo a vantagem do judeu? Ou qual a utilidade da circuncisão?
2 Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
Muita, em toda a maneira, porque, quanto ao primeiro, as palavras de Deus lhe foram confiadas,
3 Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
Pois que? Se alguns foram incrédulos, a sua incredulidade aniquilará a fé de Deus?
4 La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
De maneira nenhuma; antes seja Deus verdadeiro, e todo o homem mentiroso; como está escrito: Para que sejas justificado em tuas palavras, e venças quando fores julgado.
5 Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
E, se a nossa injustiça recomendar a justiça de Deus, que diremos? Porventura será Deus injusto, trazendo ira sobre nós? ( falo como homem)
6 La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
De maneira nenhuma: de outro modo, como julgará Deus o mundo?
7 Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
Porque, se pela minha mentira abundou mais a verdade de Deus para glória sua, porque sou ainda julgado também como pecador?
8 Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
E não dizemos (como somos blasfemados, e como alguns dizem que dizemos): Façamos males, para que venham bens: cuja condenação é justa.
9 Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
Pois que? Somos nós mais excelentes? de maneira nenhuma, pois já de antes demonstramos que, tanto judeus como gregos, todos estão debaixo do pecado;
10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
Como está escrito: Não há justo, nem ainda um:
11 Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
Não há ninguém que entenda; não há ninguém que busque a Deus:
12 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
Todos se extraviaram, e juntamente se fizeram inúteis. Não há quem faça o bem, não há nem um só
13 “Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
A sua garganta é um sepulcro aberto: com as suas línguas tratam enganosamente: peçonha de áspides está debaixo de seus lábios:
14 “Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
Cuja boca está cheia de maldição e amargura:
15 “Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
Os seus pés são ligeiros para derramar sangue:
16 maangamizi na taabu viko katika njia zao,
Em seus caminhos há destruição e miséria:
17 wala njia ya amani hawaijui.”
E não conheceram o caminho da paz:
18 “Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
Não há temor de Deus diante de seus olhos.
19 Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
Ora, nós sabemos que tudo o que a lei diz aos que estão debaixo da lei o diz, para que toda a boca se feche e todo o mundo seja condenável diante de Deus.
20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
Por isso nenhuma carne será justificada diante dele pelas obras da lei, porque pela lei vem o conhecimento do pecado.
21 Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
Mas agora se manifestou sem a lei a justiça de Deus, tendo o testemunho da lei e dos profetas;
22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
Isto é, a justiça de Deus pela fé de Jesus Cristo para todos e sobre todos os que crêem; porque não há diferença,
23 kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
Porque todos pecaram e destituídos estão da glória de Deus;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
Sendo justificados gratuitamente pela sua graça, pela redenção que há em Cristo Jesus:
25 Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
Ao qual Deus propôs para propiciação pela fé no seu sangue, para demonstração da sua justiça, pela remissão dos pecados de antes cometidos, sob a paciência de Deus;
26 Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
Para demonstração da sua justiça neste tempo presente, para que ele seja justo e justificador daquele que tem fé em Jesus.
27 Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
Onde está logo a jactância? É excluída. Por qual lei? Das obras? Não; mas pela lei da fé
28 Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
Concluímos pois que o homem é justificado pela fé sem as obras da lei.
29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
Deus é porventura somente dos judeus? E não o é também dos gentios? também dos gentios, certamente.
30 Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
Porque há um só Deus que justificará pela fé a circuncisão, e pela fé a incircuncisão.
31 Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.
Anulamos, pois, a lei pela fé? De maneira nenhuma, antes estabelecemos a lei.

< Warumi 3 >