< Warumi 3 >

1 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
quid ergo amplius est Iudaeo aut quae utilitas circumcisionis
2 Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
multum per omnem modum primum quidem quia credita sunt illis eloquia Dei
3 Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
quid enim si quidam illorum non crediderunt numquid incredulitas illorum fidem Dei evacuabit absit
4 La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
est autem Deus verax omnis autem homo mendax sicut scriptum est ut iustificeris in sermonibus tuis et vincas cum iudicaris
5 Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
si autem iniquitas nostra iustitiam Dei commendat quid dicemus numquid iniquus Deus qui infert iram secundum hominem dico
6 La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
absit alioquin quomodo iudicabit Deus mundum
7 Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
si enim veritas Dei in meo mendacio abundavit in gloriam ipsius quid adhuc et ego tamquam peccator iudicor
8 Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
et non sicut blasphemamur et sicut aiunt nos quidam dicere faciamus mala ut veniant bona quorum damnatio iusta est
9 Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
quid igitur praecellimus eos nequaquam causati enim sumus Iudaeos et Graecos omnes sub peccato esse
10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
sicut scriptum est quia non est iustus quisquam
11 Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
non est intellegens non est requirens Deum
12 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
omnes declinaverunt simul inutiles facti sunt non est qui faciat bonum non est usque ad unum
13 “Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
sepulchrum patens est guttur eorum linguis suis dolose agebant venenum aspidum sub labiis eorum
14 “Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
quorum os maledictione et amaritudine plenum est
15 “Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
veloces pedes eorum ad effundendum sanguinem
16 maangamizi na taabu viko katika njia zao,
contritio et infelicitas in viis eorum
17 wala njia ya amani hawaijui.”
et viam pacis non cognoverunt
18 “Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
non est timor Dei ante oculos eorum
19 Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
scimus autem quoniam quaecumque lex loquitur his qui in lege sunt loquitur ut omne os obstruatur et subditus fiat omnis mundus Deo
20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
quia ex operibus legis non iustificabitur omnis caro coram illo per legem enim cognitio peccati
21 Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
nunc autem sine lege iustitia Dei manifestata est testificata a lege et prophetis
22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
iustitia autem Dei per fidem Iesu Christi super omnes qui credunt non enim est distinctio
23 kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
omnes enim peccaverunt et egent gloriam Dei
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
iustificati gratis per gratiam ipsius per redemptionem quae est in Christo Iesu
25 Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
quem proposuit Deus propitiationem per fidem in sanguine ipsius ad ostensionem iustitiae suae propter remissionem praecedentium delictorum
26 Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
in sustentatione Dei ad ostensionem iustitiae eius in hoc tempore ut sit ipse iustus et iustificans eum qui ex fide est Iesu
27 Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
ubi est ergo gloriatio exclusa est per quam legem factorum non sed per legem fidei
28 Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
arbitramur enim iustificari hominem per fidem sine operibus legis
29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
an Iudaeorum Deus tantum nonne et gentium immo et gentium
30 Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
quoniam quidem unus Deus qui iustificabit circumcisionem ex fide et praeputium per fidem
31 Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.
legem ergo destruimus per fidem absit sed legem statuimus

< Warumi 3 >