< Warumi 3 >
1 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
Quel est donc l'avantage du Juif, ou quel est le profit de la Circoncision?
2 Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
[Il est] grand en toute manière; surtout en ce que les oracles de Dieu leur ont été confiés.
3 Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
Car qu'est-ce, si quelques-uns n'ont point cru? leur incrédulité anéantira-t-elle la fidélité de Dieu?
4 La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
Non sans doute! mais que Dieu soit véritable, et tout homme menteur; selon ce qui est écrit: afin que tu sois trouvé juste en tes paroles, et que tu aies gain de cause quand tu es jugé.
5 Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
Or si notre injustice recommande la justice de Dieu, que dirons-nous? Dieu est-il injuste quand il punit? ( je parle en homme.)
6 La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
Non sans doute! autrement, comment Dieu jugera-t-il le monde?
7 Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
Et si la vérité de Dieu est par mon mensonge plus abondante pour sa gloire, pourquoi suis-je encore condamné comme pécheur?
8 Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
Mais plutôt, selon que nous sommes blâmés, et que quelques-uns disent que nous disons: pourquoi ne faisons-nous du mal, afin qu'il en arrive du bien? desquels la condamnation est juste.
9 Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
Quoi donc! sommes-nous plus excellents? Nullement. Car nous avons ci-devant convaincu que tous, tant Juifs que Grecs, sont assujettis au péché.
10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
Selon qu'il est écrit: il n'y a point de juste, non pas même un seul.
11 Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
Il n'y a personne qui ait de l'intelligence, il n'y a personne qui recherche Dieu.
12 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
Ils se sont tous égarés, ils se sont tous ensemble rendus inutiles: il n'y en a aucun qui fasse le bien, non pas même un seul.
13 “Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
C'est un sépulcre ouvert que leur gosier; ils ont frauduleusement usé de leurs langues, il y a du venin d'aspic sous leurs lèvres.
14 “Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
Leur bouche est pleine de malédiction et d'amertume.
15 “Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
Leurs pieds sont légers pour répandre le sang.
16 maangamizi na taabu viko katika njia zao,
La destruction et la misère sont dans leurs voies.
17 wala njia ya amani hawaijui.”
Et ils n'ont point connu la voie de la paix.
18 “Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
La crainte de Dieu n'est point devant leurs yeux.
19 Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
Or nous savons que tout ce que la Loi dit, elle le dit à ceux qui sont sous la Loi, afin que toute bouche soit fermée, et que tout le monde soit coupable devant Dieu.
20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
C'est pourquoi nulle chair ne sera justifiée devant lui par les œuvres de la Loi: car par la Loi [est donnée] la connaissance du péché.
21 Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
Mais maintenant la justice de Dieu est manifestée sans la Loi, lui étant rendu témoignage par la Loi, et par les Prophètes.
22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
La justice, dis-je, de Dieu par la foi en Jésus-Christ, s'étend à tous et sur tous ceux qui croient;
23 kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
car il n'y a nulle différence, vu que tous ont péché, et qu'ils sont entièrement privés de la gloire de Dieu.
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
Etant justifiés gratuitement par sa grâce, par la rédemption qui est en Jésus-Christ;
25 Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
Lequel Dieu a établi de tout temps pour [être une victime] de propitiation par la foi, en son sang, afin de montrer sa justice, par la rémission des péchés précédents, selon la patience de Dieu;
26 Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
Pour montrer, [dis-je], sa justice dans le temps présent, afin qu'il soit [trouvé] juste, et justifiant celui qui est de la foi de Jésus.
27 Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
Où est donc le sujet de se glorifier? Il est exclu. Par quelle Loi? [est-ce par la Loi] des œuvres? Non, mais par la Loi de la foi.
28 Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
Nous concluons donc que l'homme est justifié par la foi, sans les œuvres de la Loi.
29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
[Dieu] est-il seulement le Dieu des Juifs? ne l'est-il pas aussi des Gentils? certes il l'est aussi des Gentils.
30 Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
Car il y a un seul Dieu qui justifiera par la foi la Circoncision, et le Prépuce [aussi] par la foi.
31 Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.
Anéantissons-nous donc la Loi par la foi? Non sans doute! mais au contraire, nous affermissons la Loi.