< Warumi 3 >
1 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
What then is the advantage of the Jew, or what is the profit of circumcision?
2 Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
Much, every way: chiefly, because they were intrusted with the oracles of God.
3 Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
For what if some did not believe? shall their incredulity make the faithfulness of God of no effect?
4 La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
God forbid: yea, let God be acknowledged true, though every man be a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy words, and mightest overcome, when thou judgest.
5 Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
"But if our unrighteousness confirm the righteousness of God, what shall we say? Is not God unrighteous, who inflicteth his wrath?" (I speak as a man) God forbid:
6 La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
for then how shall God judge the world?
7 Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
"But, say you, if the truth of God hath abounded unto his glory through my falshood, why yet am I also judged as a sinner?
8 Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
and why may we not do evil that good may come?"---as we are injuriously charged, and as some affirm that we say; whose condemnation is just.
9 Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
"What then are we the better?" Not at all, in point of justification; for we have before proved that both Jews and Gentiles are all under sin: as it is written,
10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
"There is none righteous, no not one;
11 Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
there is none that understandeth; there is none that seeketh after God.
12 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
They are all gone out of the way, they are become unprofitable, there is none that practiseth goodness, no not one.
13 “Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
Their throat is an open sepulchre: with their tongues they have used deceit; the poison of asps is under their lips:
14 “Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
whose mouth is full of cursing and bitterness:
15 “Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
their feet are swift to shed blood:
16 maangamizi na taabu viko katika njia zao,
destruction and misery are in their ways:
17 wala njia ya amani hawaijui.”
and the way of peace they have not known; and the fear of God is not before their eyes."
18 “Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
Now we know that whatsoever the law saith,
19 Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
it saith to those under the law: that every mouth may be stopped, and all the world obnoxious to the justice of God.
20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
Wherefore by the works of the law no flesh shall be justified before Him: for by the law is the knowledge of sin.
21 Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
But now, without the law, righteousness before God is manifested, being attested by the law and the prophets;
22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
and this righteousness of God is by faith in Jesus Christ unto all and upon all believers; for there is no difference;
23 kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
for all have sinned and come short of the glory of God;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
being justified freely by his grace, because of the redemption that is in Christ Jesus:
25 Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
whom God hath appointed to be a propitiation, through faith in his blood, for a demonstration of his righteousness, in the remission of past sins, according to the forbearance of God;
26 Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
for a demonstration, I say, of his righteousness at this time: that He might be just, and the justifier of him, that believeth in Jesus.
27 Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
Where then is boasting? it is excluded: by what law? of works? no: but by the law of faith.
28 Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
Therefore we conclude, that a man is justified by faith, without the works of the law:
29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
or is He the God of the Jews only, and not also of the Gentiles?
30 Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
surely of the Gentiles also: seeing it is one God who will justify the circumcision by faith, and uncircumcision also through faith.
31 Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.
Do we then make the law of none effect through faith? God forbid: yea we establish the law.