< Warumi 3 >

1 Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
What advantage then hath the Jew? or what is the profit of circumcision?
2 Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
Much every way: first of all, that they were intrusted with the oracles of God.
3 Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
For what if some were without faith? shall their want of faith make of none effect the faithfulness of God?
4 La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
God forbid: yea, let God be found true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy words, And mightest prevail when thou comest into judgment.
5 Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
But if our unrighteousness commendeth the righteousness of God, what shall we say? Is God unrighteous who visiteth with wrath? (I speak after the manner of men.)
6 La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
God forbid: for then how shall God judge the world?
7 Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
But if the truth of God through my lie abounded unto his glory, why am I also still judged as a sinner?
8 Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
and why not (as we be slanderously reported, and as some affirm that we say), Let us do evil, that good may come? whose condemnation is just.
9 Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
What then? are we in worse case than they? No, in no wise: for we before laid to the charge both of Jews and Greeks, that they are all under sin;
10 Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
as it is written, There is none righteous, no, not one;
11 Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
There is none that understandeth, There is none that seeketh after God;
12 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
They have all turned aside, they are together become unprofitable; There is none that doeth good, no, not so much as one:
13 “Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
Their throat is an open sepulchre; With their tongues they have used deceit: The poison of asps is under their lips:
14 “Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
Whose mouth is full of cursing and bitterness:
15 “Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
Their feet are swift to shed blood;
16 maangamizi na taabu viko katika njia zao,
Destruction and misery are in their ways;
17 wala njia ya amani hawaijui.”
And the way of peace have they not known:
18 “Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
There is no fear of God before their eyes.
19 Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
Now we know that what things soever the law saith, it speaketh to them that are under the law; that every mouth may be stopped, and all the world may be brought under the judgment of God:
20 Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
because by the works of the law shall no flesh be justified in his sight: for through the law [cometh] the knowledge of sin.
21 Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
But now apart from the law a righteousness of God hath been manifested, being witnessed by the law and the prophets;
22 Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
even the righteousness of God through faith in Jesus Christ unto all them that believe; for there is no distinction;
23 kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
for all have sinned, and fall short of the glory of God;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
25 Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
whom God set forth [to be] a propitiation, through faith, by his blood, to shew his righteousness, because of the passing over of the sins done aforetime, in the forbearance of God;
26 Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
for the shewing, [I say], of his righteousness at this present season: that he might himself be just, and the justifier of him that hath faith in Jesus.
27 Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
Where then is the glorying? It is excluded. By what manner of law? of works? Nay: but by a law of faith.
28 Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
We reckon therefore that a man is justified by faith apart from the works of the law.
29 Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
Or is God [the God] of Jews only? is he not [the God] of Gentiles also? Yea, of Gentiles also:
30 Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
if so be that God is one, and he shall justify the circumcision by faith, and the uncircumcision through faith.
31 Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.
Do we then make the law of none effect through faith? God forbid: nay, we establish the law.

< Warumi 3 >