< Warumi 2 >
1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
Therefore inexcusable you are, O man everyone you who [are] judging; In that which for you judge the other, yourself you are condemning; for the same things you do who are judging.
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
We know however that the judgment of God is according to truth upon those such things practicing;
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
Suppose you now this, O man you who [are] judging those such things practicing and doing them [yourself], that you yourself will escape the judgment of God?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or the riches of the kindness of Him and the forbearance and the patience despise you not knowing that the kindness of God to repentance you leads?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
Because of however the hardness of you and unrepentant heart you are treasuring up to yourself wrath in [the] day of wrath and revelation (and *O*) of justice of God,
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
who will give to each according to the works of him,
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
to those who indeed with endurance in work good glory and honor and immortality are seeking life eternal; (aiōnios )
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
to those however of self-interest and disobeying (indeed *k*) the truth, being persuaded about however unrighteousness, wrath and anger
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
tribulation and distress upon every soul of man which is working the evil, of Jew both first and also of Greek;
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
glory however and honor and peace to everyone who is doing good, to Jew both first and to Greek;
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
Not for there is partiality with God.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
As many as for without [the] Law have sinned, without [the] Law also will perish; and as many as in [the] Law have sinned, through [the] Law will be judged;
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
not for the hearers (*k*) of [the] law [are] righteous with God, but the doers (*k*) of [the] law will be justified.
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
When for Gentiles not the law having by nature the [things] of the law (they may do, *N(k)O*) these [the] Law not having to themselves are a law,
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
who show the work of the law written in the hearts when they are bearing witness to them their conscience and between one another the thoughts accusing or also presenting a defense
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
on day (when *NK(o)*) (judges *N(k)O*) God the secrets of men according to the gospel of mine through Christ Jesus.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
(If *N(K)O*) (however *no*) you yourself a Jew are called and you rely on (the *k*) law and you boast in God
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
and know the will and approve the [things] being superior being instructed out of the law;
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
you are confident then [that] you yourself a guide being of [the] blind, a light to those in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
an instructor of [the] foolish, a teacher of infants, having the embodiment of knowledge and of the truth in the law;
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
You who [are] then teaching another yourself not do you teach? You who [are] preaching not to steal do you steal?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
You who [are] saying not to commit adultery do you commit adultery? You who [are] abhorring idols do you rob temples?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
You who in law boast, through the transgression of the law God dishonor you?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For the name of God through you is blasphemed among the Gentiles even as it has been written.
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
Circumcision indeed for profits if [the] law you shall do; if however a transgressor of law you shall be, the circumcision of you uncircumcision has become.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
If therefore the uncircumcision the requirements of the law shall keep, (surely *N(k)O*) the uncircumcision of him for circumcision will be reckoned?
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
And will judge the by nature uncircumcision the law fulfilling you who with [the] letter and circumcision [are] a transgressor of law.
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
Not for the [one] on the outward a Jew is, neither the [one] outwardly the outward in flesh [is] circumcision,
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
but he who [is] on the inward a Jew [is one], and circumcision [is] of heart in spirit not in letter, of whom the praise [is] not of men but of God.