< Warumi 2 >
1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
Wherefore thou art without excuse, O man that judgest, whoever thou art. For wherein thou judgest another, thou condemnest thyself; for thou that judgest doest the same things.
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
But we know that the judgment of God is according to truth against those who practise such things.
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
And dost thou suppose, O man, who art judging those who do such things, and art thyself doing the same, that thou wilt escape the judgment of God?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or dost thou despise the riches of his goodness and forbearance and longsuffering, not knowing that the goodness of God is leading thee to repentance?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
But according to thy hardness and impenitent heart, thou art treasuring up for thyself wrath against the day of wrath and of the manifestation of the righteous judgment of God,
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
who will render to every one according to his works;
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
everlasting life to those who by patient continuance in well-doing seek for glory, and honor, and incorruption; (aiōnios )
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
but to those who are contentious, and disobedient to the truth; but obey unrighteousness, there will be wrath and indignation.
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
Tribulation and distress will be upon every soul of man whose works are evil, of the Jew first, and also of the Greek;
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
but glory, honor, and peace, to every one whoso works are good, to the Jew first, and also to the Greek.
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
For there is no respect of persons with God.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
For as many as have sinned without a law, will also perish without a law; and as many as have sinned under a law, will be judged by a law,
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
for it is not the hearers of a law who are righteous before God, but the doers of a law will be accounted righteous; —
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
for when the gentiles, who have no law, do by nature what is required by the Law, these, having no law, are a law to themselves;
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
since they show that what the Law requireth is written in their hearts, their conscience bearing witness, and their thoughts in turn accusing or defending them; —
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
in the day when God shall judge the secrets of men by Jesus Christ, according to the gospel which I have preached.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
But if thou art called a Jew, and restest on the Law, and makest thy boast of God,
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
and knowest his will, and approvest the things that are more excellent, being instructed out of the Law;
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
and art confident that thou thyself art a guide of the blind, a light to those who are in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
an instructor of those who lack wisdom, a teacher of babes, having the form of knowledge and of the truth in the Law, —
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
dost thou then who teachest another, not teach thyself? Thou who proclaimest that others should not steal, dost thou steal?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
Dost thou who forbiddest to commit adultery, thyself commit adultery? Thou that abhorrest idols, dost thou rob temples?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
Dost thou who boastest of the Law, dishonor God by breaking the Law?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For, as it is written, “the name of God is on your account blasphemed among the gentiles.”
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
For circumcision is indeed a benefit to thee, if thou keep the Law; but if thou art a breaker of the Law, thy circumcision hath become uncircumcision.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
If then he who is uncircumcised keep the precepts of the Law, shall not he though uncircumcised be regarded as circumcised?
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
Yea, those who are by nature uncircumcised, if they perform the law, will judge thee, who having a written Law and circumcision, art a breaker of the Law.
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
For he is not a Jew, who is one outwardly, nor is that circumcision, which is outward, in the flesh;
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
but he is a Jew who is one inwardly; and circumcision is of the heart, spiritual, not literal, whose praise is not of men, but of God.