< Warumi 2 >

1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
Therefore you are inexcusable, O man, whoever you are that judge: for wherein you judge another, you condemn yourself; for you that judge do the same things.
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
But we are sure that the judgment of God is according to truth against them which commit such things.
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
And think you this, O man, that judge them which do such things, and do the same, that you shall escape the judgment of God?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or despise you the riches of his goodness and forbearance and long-suffering; not knowing that the goodness of God leads you to repentance?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
But after your hardness and impenitent heart treasure up to yourself wrath against the day of wrath and revelation of the righteous judgment of God;
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
Who will render to every man according to his deeds:
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios g166)
To them who by patient continuance in well doing seek for glory and honor and immortality, eternal life: (aiōnios g166)
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
But to them that are contentious, and do not obey the truth, but obey unrighteousness, indignation and wrath,
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
Tribulation and anguish, on every soul of man that does evil, of the Jew first, and also of the Gentile;
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
But glory, honor, and peace, to every man that works good, to the Jew first, and also to the Gentile:
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
For there is no respect of persons with God.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
For as many as have sinned without law shall also perish without law: and as many as have sinned in the law shall be judged by the law;
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
(For not the hearers of the law are just before God, but the doers of the law shall be justified.
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
For when the Gentiles, which have not the law, do by nature the things contained in the law, these, having not the law, are a law to themselves:
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
Which show the work of the law written in their hearts, their conscience also bearing witness, and their thoughts the mean while accusing or else excusing one another; )
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
In the day when God shall judge the secrets of men by Jesus Christ according to my gospel.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
Behold, you are called a Jew, and rest in the law, and make your boast of God,
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
And know his will, and approve the things that are more excellent, being instructed out of the law;
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
And are confident that you yourself are a guide of the blind, a light of them which are in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
An instructor of the foolish, a teacher of babes, which have the form of knowledge and of the truth in the law.
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
You therefore which teach another, teach you not yourself? you that preach a man should not steal, do you steal?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
You that say a man should not commit adultery, do you commit adultery? you that abhor idols, do you commit sacrilege?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
You that make your boast of the law, through breaking the law dishonor you God?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For the name of God is blasphemed among the Gentiles through you, as it is written.
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
For circumcision truly profits, if you keep the law: but if you be a breaker of the law, your circumcision is made uncircumcision.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
Therefore if the uncircumcision keep the righteousness of the law, shall not his uncircumcision be counted for circumcision?
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
And shall not uncircumcision which is by nature, if it fulfill the law, judge you, who by the letter and circumcision do transgress the law?
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
For he is not a Jew, which is one outwardly; neither is that circumcision, which is outward in the flesh:
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
But he is a Jew, which is one inwardly; and circumcision is that of the heart, in the spirit, and not in the letter; whose praise is not of men, but of God.

< Warumi 2 >