< Warumi 2 >
1 Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
For which reason, you are without excuse, O man, whoever you are, that judge; for in that in which you judge another, you condemn yourself; for you who judge, practice the same things.
2 Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
But we know that the judgment of God against those who practice such things, is according to truth.
3 Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
But do you, O man, who judge those that practice such things, and yet do the same, conclude that you will escape the judgment of God?
4 Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
Or, do you despise the riches of his goodness, and his forbearance, and his long suffering, not knowing that the goodness of God leads you to repentance?
5 Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
But, according to your hard and impenitent heart, you treasure up to yourself wrath for a day of wrath, and of the revelation of the righteous judgment of God,
6 Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
who will render to every man according to his works;
7 Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
to those who, by patient continuance in good works, seek for glory and honor and incorruptibility, eternal life: (aiōnios )
8 Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
but to those who are contentious, and obey not the truth, but obey unrighteousness, anger and wrath,
9 Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
affliction and distress, upon every soul of man that practices what is evil, of the Jew first, and also of the Greek:
10 bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
but glory and honor and peace to every one that practices what is good, to the Jew first, and also to the Greek:
11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
for there is no respect of persons with God.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
For as many as have sinned without law, shall also perish without law; and as many as have sinned under law, shall be judged by law,
13 Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
in the day when God shall judge the secret works of men by Jesus Christ, according to my gospel.
14 (Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
For not the hearers of the law are just before God, but the doers of the law shall be justified.
15 Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
For when the Gentiles, who have not a law, do, by nature, the things of the law, these who have not a law, are a law to themselves,
16 Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
who show that the work which the law requires, is written in their hearts, their conscience bearing testimony, and their reasonings with each other accusing, or making excuse.
17 Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
But if you are named Jew, and rest in the law, and make your boast in God.
18 kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
and know his will, and approve what is excellent, being instructed by the law:
19 kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
if you are also confident that you yourself are a guide for the blind, a light to those who are in darkness,
20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
an instructor of the simple, a teacher of the unlearned, because you have the form of true knowledge in the law;
21 basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
you, then, who teach another, do you not teach yourself? You who preach that a man should not steal, do you steal?
22 Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
You who say that a man should not commit adultery, do you commit adultery? You who detest idols, do you rob temples?
23 Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
You who make your boast in the law, do you, by transgressing the law, dishonor God?
24 Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
For the name of God is reviled among the Gentiles, on account of you, as it is written.
25 Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
Now, circumcision is indeed profitable, if you keep the law: but, if you transgress the law, your circumcision becomes uncircumcision.
26 Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
If, then, he who is uncircumcised keeps the righteousness of the law, shall not his uncircumcision be counted for circumcision?
27 Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
And shall not he whose want of circumcision is owing to his birth, if he keeps the law, condemn you, who, by the literal circumcision, transgress the law?
28 Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
For he is not a Jew who is one outwardly, nor is that circumcision which is outward in the flesh:
29 Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.
but he is a Jew who is one inwardly; and circumcision is that of the heart, in the spirit, not in the letter, whose praise is not of men, but of God.