< Warumi 16 >

1 Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
Je vous recommande Phébé, notre soeur, qui est diaconesse de l'église de Cenchrées,
2 Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
afin que vous la receviez, en notre Seigneur, d'une manière digne des saints, et que vous l'assistiez dans toute affaire, où elle pourrait avoir besoin de vous; car elle a été elle-même la protectrice de bien des frères, et la mienne en particulier.
3 Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
Saluez Prisca et Aquilas, mes compagnons d'oeuvre en Jésus-Christ,
4 Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
qui ont exposé leur tête pour me sauver la vie: ce n'est pas moi seul qui leur rends grâces, mais ce sont aussi toutes les églises des Gentils.
5 Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
Saluez aussi rassemblée qui se réunit dans leur maison. Saluez mon cher Épénète, qui a été les prémices de l'Asie, pour Christ.
6 Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
Saluez Marie, qui a beaucoup travaillé pour vous.
7 Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
Saluez Andronicus et Junias, mes parents et mes compagnons de captivité, qui sont avantageusement connus des apôtres, et qui se sont attachés à Christ, même avant moi.
8 Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
Saluez Amplias qui m'est cher dans le Seigneur.
9 Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
Saluez Urbain notre compagnon d’oeuvre en Christ, ainsi que mon cher Stachys.
10 Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
Saluez Apelle qui a fait ses preuves, en Christ. Saluez les gens de la maison d'Aristobule.
11 Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
Saluez Hérodion, mon parent. Saluez ceux de la maison de Narcisse qui sont au Seigneur.
12 Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
Saluez Tryphène et Tryphose, car elles ont travaillé pour le Seigneur. Saluez notre chère Perside; elle a beaucoup travaillé pour le Seigneur.
13 Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
Saluez Rufus, l'élu dans le Seigneur, et sa mère, que je regarde comme la mienne.
14 Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
Saluez Asyncritus, Phlégon, Hermès, Patrobas, Hermasetles frères qui sont avec eux.
15 Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
Saluez Philologue et Julie, Nérée et sa soeur, ainsi qu'Olympas et tous les saints qui sont avec eux.
16 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
Saluez-vous les uns les autres par un saint baiser. Toutes les églises de Christ vous saluent.
17 Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
Je vous invite, mes frères, à bien avoir l'oeil sur ceux qui causent les dissensions et les chutes par leur opposition à l’enseignement que vous avez reçu. Eloignez-vous d'eux;
18 Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
car de telles gens ne servent point Christ, notre Seigneur, mais ils sont les serviteurs de leur ventre, et avec leurs bonnes paroles et leur langage flatteur, ils trompent les coeurs des innocents.
19 Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
Je vous y invite, car votre soumission est parvenue aux oreilles de tout le monde; je me réjouis donc à votre sujet, mais je désire que vous soyez habiles pour le bien, tout en étant innocents pour le mal.
20 Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
Le Dieu de paix écrasera promptement Satan sous vos pieds. Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous!
21 Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
Timothée, le compagnon de mes travaux, vous salue; Lucius, Jason et Sosipatros, mes parents, vous saluent aussi.
22 Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
Je vous salue dans le Seigneur, moi Tertius, qui écris cette lettre.
23 Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
Gaïus mon hôte et celui de toute l'église, vous salue. Éraste, le trésorier de la ville, et notre frère Quartus, vous saluent.
24 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous tous! Amen!
25 Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios g166)
A Celui qui peut vous affermir dans mon évangile et dans la prédication qui se fait de Jésus-Christ — conformément à la révélation du mystère celé durant de longs siècles, (aiōnios g166)
26 Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios g166)
mais révélé maintenant, ainsi que par les écrits des Prophètes, sur l'ordre du Dieu éternel, pour amener à l'obéissance de la foi toutes les nations — (aiōnios g166)
27 Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
à Dieu, seul sage, soit la gloire aux siècles des siècles, par Jésus-Christ! Amen! (aiōn g165)

< Warumi 16 >