< Warumi 16 >
1 Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
I commend unto you Phoebe our sister, who is a servant of the church that is at Cenchreae:
2 Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
that ye receive her in the Lord, worthily of the saints, and that ye assist her in whatsoever matter she may have need of you: for she herself also hath been a succourer of many, and of mine own self.
3 Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
Salute Prisca and Aquila my fellow-workers in Christ Jesus,
4 Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
who for my life laid down their own necks; unto whom not only I give thanks, but also all the churches of the Gentiles:
5 Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
and [salute] the church that is in their house. Salute Epaenetus my beloved, who is the firstfruits of Asia unto Christ.
6 Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
Salute Mary, who bestowed much labour on you.
7 Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
Salute Andronicus and Junias, my kinsmen, and my fellow-prisoners, who are of note among the apostles, who also have been in Christ before me.
8 Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
Salute Ampliatus my beloved in the Lord.
9 Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
Salute Urbanus our fellow-worker in Christ, and Stachys my beloved.
10 Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
Salute Apelles the approved in Christ. Salute them which are of the [household] of Aristobulus.
11 Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
Salute Herodion my kinsman. Salute them of the [household] of Narcissus, which are in the Lord.
12 Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
Salute Tryphaena and Tryphosa, who labour in the Lord. Salute Persis the beloved, which laboured much in the Lord.
13 Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
Salute Rufus the chosen in the Lord, and his mother and mine.
14 Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
Salute Asyncritus, Phlegon, Hermes, Patrobas, Hermas, and the brethren that are with them.
15 Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
Salute Philologus and Julia, Nereus and his sister, and Olympas, and all the saints that are with them.
16 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
Salute one another with a holy kiss. All the churches of Christ salute you.
17 Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
Now I beseech you, brethren, mark them which are causing the divisions and occasions of stumbling, contrary to the doctrine which ye learned: and turn away from them.
18 Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
For they that are such serve not our Lord Christ, but their own belly; and by their smooth and fair speech they beguile the hearts of the innocent.
19 Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
For your obedience is come abroad unto all men. I rejoice therefore over you: but I would have you wise unto that which is good, and simple unto that which is evil.
20 Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
And the God of peace shall bruise Satan under your feet shortly. The grace of our Lord Jesus Christ be with you.
21 Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
Timothy my fellow-worker saluteth you; and Lucius and Jason and Sosipater, my kinsmen.
22 Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
I Tertius, who write the epistle, salute you in the Lord.
23 Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
Gaius my host, and of the whole church, saluteth you. Erastus the treasurer of the city saluteth you, and Quartus the brother.
24 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
25 Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios )
Now to him that is able to stablish you according to my gospel and the preaching of Jesus Christ, according to the revelation of the mystery which hath been kept in silence through times eternal, (aiōnios )
26 Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios )
but now is manifested, and by the scriptures of the prophets, according to the commandment of the eternal God, is made known unto all the nations unto obedience of faith; (aiōnios )
27 Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn )
to the only wise God, through Jesus Christ, to whom be the glory for ever. Amen. (aiōn )