< Warumi 16 >

1 Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
I recommend to you Phebe, our sister, who is a deaconess of the congregation at Cenchrea,
2 Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
that you may receive her in the Lord, as becomes saints, and assist her, in whatever business she may have need of you: for, indeed, she has been a helper of many, and especially of me.
3 Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
Salute Priscilla and Aquila, my fellow-laborers in Christ Jesus.
4 Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
These persons, for my life, laid down their own neck; to whom not only I give thanks, but even all the congregations of the Gentiles.
5 Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
Likewise, salute the congregation which is in their house. Salute Epenetus, my beloved, who is the first fruit of Asia to Christ.
6 Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
Salute Mary, who labored much for us.
7 Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
Salute Andronicus, and Junias, my kinsmen, and my fellow-prisoners, who are of note among the Apostles, and who were in Christ before me.
8 Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
Salute Amplias, my beloved in the Lord.
9 Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
Salute Urbanas, our fellow-laborer in Christ, and Stachys, my beloved.
10 Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
Salute Appelles, the approved in Christ. Salute those who are of the family of Aristobulus.
11 Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
Salute Herodion, my kinsman. Salute those of the family of Narcissus, who are in the Lord.
12 Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
Salute Tryphena and Tryphosa, who labor in the Lord. Salute the beloved Persis, who labored much in the Lord.
13 Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
Salute Rufus, the chosen in the Lord, and her who is the mother both of him and of me.
14 Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
Salute Asyncritus, Phlegon, Hermas, Patrobas, Hermes, and the brethren with them.
15 Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
Salute Philologus, and Julia, Nereus, and his sister, and Olympas, and all the saints who are with them.
16 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
Salute one another with a holy kiss. The congregations of Christ salute you.
17 Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
Now, I beseech you, brethren, mark them who make separations and occasions of falling, contrary to the doctrine which you have learned; and avoid them.
18 Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
For they who are such, do not serve out Lord Jesus, but their own belly; and by flattery and fair speeches, deceive the hearts of the simple.
19 Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
Now your obedience is reported to all men. I therefore rejoice on your account; nevertheless, I wish you, indeed, to be wise with respect to good; and simple with respect to evil.
20 Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
May the God of peace bruise Satan under your feet soon! The favor of our Lord Jesus Christ be with you.
21 Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
Timothy, my fellow-laborer, and Lucius, and Jason, and Sosipater, my kinsmen, salute you.
22 Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
I, Tertius, who wrote this letter, salute you in the Lord.
23 Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
Gaius, my host, and of the whole congregation, salutes you. Erastus, the chamberlain of the city, salutes you, and Quartus, your brother.
24 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
The favor of our Lord Jesus Christ be with you all! Amen.
25 Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios g166)
Now to Him who is able to establish you according to my gospel, and the proclamation of Jesus Christ, according to the revelation of the secret, concealed in the times of the ages, (aiōnios g166)
26 Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios g166)
(but is now made manifest by the prophetic writings, and by the commandment of the eternal God is made known to all the Gentiles, in order to the obedience of faith: ) (aiōnios g166)
27 Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn g165)
to the wise God alone, through Jesus Christ, to whom be the glory forever. Amen. (aiōn g165)

< Warumi 16 >